Saturday, July 4, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

JINSI ANJELLAH ALIVYOONGEZA UTAMU, USHINDANI BONGO FLEVA

VIPIGO vya baba yake vilimuongezea nguvu ya kufanya muziki kwa bidii

admin by admin
March 15, 2021
in MAKALA-BURUDANI
0
JINSI ANJELLAH ALIVYOONGEZA UTAMU, USHINDANI BONGO FLEVA

Na AMINA KASHEBA

MACHI 10, mwaka huu ilikuwa ni siku ya kipekee kwa nyota mpya wa muziki wa Bongo Fleva, Angelina George ‘Anjellah’.

Anjellah ni ingizo jipya katika muziki huo kupitia lebo ya Konde Gang inayomilikiwa na Rajabu Kahali ‘Harmonize’.

Msanii huyo aliyesota kupata ulaji kwa wasanii wakubwa wanaomiliki lebo zenye ushindani mkubwa nchini, hatimaye alikula shavu baada ya kuonwa na Harmonize akiwa mtaani akiimba kwa kurudia nyimbo za wasanii mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Ili kuonyesha kuwa Harmonize hakubahatisha kumpa nafasi Anjellah katika lebo yake, alimtambulisha kwa kuimba naye nyimbo ya ‘All Night’ ikiwa ni nyimbo yake ya kwanza kabla ya kumthibitisha katika lebo yake.

Hatimaye mwishoni mwa wiki iliyopita, lebo ya Konde Gang ilimkaribisha na kumtambulisha rasmi msanii huyo katika hafla iliyofanyika makao makuu ya studio za Harmonize.

Hapo ndipo safari rasmi ya Anjella ilipoanza, alipanda jukwaani kutumbuiza nyimbo mbalimbali za wasanii wengine kabla ya kuimba nyimbo yake mpya.

Huku akishangiliwa na mamia ya mashabiki waliojitokeza katika utambulisho huo, Anjella alitambulisha singo ya ‘Kama’.

Singo hiyo ya imekuja mwezi mmoja baada ya kutoka na kibao cha All Night alichoshirikiana na Harmonize.

Kuingia katika muziki kwa msanii huyo ni dhahiri kuwa kumezidi kuongeza ushindani wa wanawake katika muziki huo pendwa Afrika Mashariki na Kati.

Akizungumza baada ya kutambulishwa, Anjellah  alisema moja ya malengo yake ni kuwa miongoni mwa wasanii bora wa kike wanaotambulika Afrika jamabo ambalo ni rahisi kulifikia baada ya kujiunga na lebo kubwa nchini.

“Nimehaingaika sana hadi kufikia hapa nilipo leo, namshukuru Mungu, uongozi nzima wa Konde Gang chini ya Harmonize, mashabiki na Watanzania wote mliokuwa mkinipa moyo kabla sijapata nafasi hii ya kipekee ambayo wanamuziki wengi walitamani kuipata”, alisema Anjellah.

Aliongeza kuwa baada ya kupata bahati ya kuwa msanii wa kwanza katika lebo hiyo, hatabweteka kwani atahakikisha anatunga na kuimba nyimbo ambazo zitazidi kumpandisha chati na kutoa upinzani kwa wasanii wenzakewa kike.

Aidha Anjellah alieleza kuwa ataongeza bidii na maombi ili kufanikisha ndoto zale nyingi na kupata mafanikio kama ambayo wasanii wenzake wa kike waliotangulia kwenye muziki wamepata.

Mwimbaji huyo anasema kwa sasa bidii zote anaziweka katika kazi na kusikiliza watu waliotangulia katika muziki ili kupata kitu cha utofauti katika muziki.

“Unajua jambo nzuri ni kusikiliza wakubwa wako walipoita wamefanya nini hadi kufikia hapo walipo kwani lengo langu nami ni kufika mbali ikiwemo kufanya kolabo na wasanii wakubwa ndani na nje ya nchi.

“Nitahakikisha naitumia vyema nafasi niliyopata, hii ni bahati ya kipekee sana, sitaichezea wala kumdharau aliyefanikisha ndoto zangu,” aliongeza.

Msanii huyo anaongeza kwa kusema kuwa atahakikisha anafanya kazi kwa bidii na kusikiliza ushauri ambao anaamini utamuongezea ufanisi katika kazi yake.

Akizungumzia changamoto ambazo amepitia hadi kufikia sasa, Anjellah anasema kuwa alikuwa akipigwa mara kwa mara na wazazi wake pindi alipotoroka nyumbani na kwenda mitaani kuimba.

Anasema kuwa kuna wakati wazazi wake walidhani kuwa anachelewa kurudi nyumbani kwa vile alikwenda kwa mwanaume wakati ukweli ni kuwa alikuwa akipita sehemu mbalimbali kuimba kwa ajili ya kutafuta ridhiki na si vinginevyo.

“Kila nilipochelewa kurudi nyumbani baba alinipiga na kunitolea maneno makali, nilivumilia huku nikiamini kuwa ipo siku wazazi wangu wataelewa kuwa nilikuwa nikitafuta nini,” alisema.

Anasema kuwa, hata Harmonize alipomtafuta na kutaka kumtoa kimuziki hakuamini kwani hakuwahi kufikiria kama msanii mkubwa kama huyo anaweza kumpa nafasi na kufanikisha ndoto zake kwani kuna idadi kubwa ya wasanii wenye uwezo ambao angeweza kuwasaidia lakini kumbe bahati ilikuwa yake.

Aliongeza kuwa huu ndio kwannza ameanza na atahakikisha hamuangushi Harmonize wala Watanzania ambao walikuwa nyuma yake katika kipindi ambacho alikuwa anatafuta nafasi ya kuonyesha kipaji chake.

Naye Harmonize alisema hajuti na hatajutia uamuzi wa kumuingiza Anjellah katika lebo yake kwani kipaji alichonacho ni kikubwa na kitaongeza ufanisi wa lebo yake.

Harmonize alisema kuwa baada ya miezi sita Anjellah atakuwa moto wa kuotea mbali na ametenga muda mwingi kwa ajili ya kumpika na kumshindanisha na wasanii wengine wa kike nchini.

“Baada ya muda mfupi Anjellah ndiye atakuwa msanii bora wa kike nchini, namuamini na nawahakikishia wapenzi wa muziki nchini kuwa binti huyu ni moto wa kuotea mbali,” alisisitiza Harmonize.

Previous Post

Gazeti KONGWE LA UHURU, Leo MACHI 1️⃣5️⃣, 2️⃣0️⃣2️⃣1️⃣

Next Post

KAMATI YA BUNGE YAISHAURI TASAF KUWAUNGANISHA WALIOJIKWAMUA

admin

admin

Next Post
KAMATI YA BUNGE YAISHAURI TASAF KUWAUNGANISHA WALIOJIKWAMUA

KAMATI YA BUNGE YAISHAURI TASAF KUWAUNGANISHA WALIOJIKWAMUA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved