Tuesday, May 20, 2025
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English English Kiswahili Kiswahili
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • English English
  • Kiswahili Kiswahili
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result
Mwanzo MAKALA

MFAHAMU MHANDISI PATRICK MFUGALE, MWAMBA WA MADARAJA, BARABARA NCHINI

>>MADARAJA 1,400 na barabara km 36,258 ni alama isiyofutika ya maisha yake duniani

admin by admin
July 2, 2021
in MAKALA
0 0
0
MFAHAMU MHANDISI PATRICK MFUGALE, MWAMBA WA MADARAJA, BARABARA NCHINI
0
SHARES
721
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

MAISHA ya miaka 41 katika sekta ya ujenzi yametosha kujenga historia iliyotukuka ya maisha ya duniani ya Mhandisi Patrick Mfugale. 

Kile kinachoelezwa kuwa maisha yako ndiyo yatakayotafsiri kumbukumbu na alama za ulichokifanya ulimwenguni, kimeakisi uhalisia wa miaka 68 ya uhai wake.

Hata kama haukuwahi kusikia jina lake, bila shaka umepita katika moja ya miundombinu iliyojengwa kwa mchango wa taaluma na utendaji wake.

Huyu ni Mhandisi Patrick Mfugale, mwamba wa barabara na madaraja makubwa na madogo nchini, sifa hizo zinatokana na utumishi uliotukuka wa miaka 41 katika sekta ya ujenzi akishika nyadhifa mbalimbali.

Juni 14, mwaka huu, ilikuwa siku ya mwisho kuonekana hadharani akitekeleza majukumu yake, siku ambayo Rais Samia alifanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Daraja la JP Magufuli, jijini Mwanza.

Juni 29, ndiyo siku aliyoumaliza mwendo, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma, alikokimbizwa kupatiwa matibabu baada ya kuugua ghafla wakati akitekeleza majukumu yake.

Mbali na alama alizoziacha jina lake litabaki milele, kutokana na moja ya miradi aliyoshiriki utekelezaji wake kupewa Jina lake nalo ni Daraja la Mfugale linalounganisha makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere.

Historia yake kazini

Mhandisi Mfugale alianza kazi Wizara ya ujenzi tangu mwaka 1977, ambapo hadi anafariki ameacha historia ya kujenga barabara zenye urefu wa kilometa 36,258 na madaraja 1,400.

Baadhi ya waliowahi kufanyakazi naye, wanasema hakupenda kusifiwa katika utendaji wake, badala yake alishauri sifa hizo kuelekezwa kwa nchi yake.

Pia, Mhandisi Mfugale ndiye miongoni mwa wahandisi wachache walioamua kurejea nchini na kutumikia taifa baada ya kuhitimu taaluma hiyo, wakati wengi wao walitokomea nje ya nchi kufanya kazi huko.

Baadhi ya madaraja aliyosimamia na kusanifu ujenzi wake, yameingia katika orodha ya miradi 10 bora kwa urefu barani Afrika, likiwemo Daraja la JP Magufuli ambalo likikamilika litakuwa namba sita kwa urefu.

Hata hivyo Daraja la Benjamin Mkapa la Rufiji mkoani Pwani, limeingia kuwa namba tisa kwa urefu Afrika.

Pamoja na madaraja hayo mengine makubwa aliyosimamia ujenzi wake tangu alipokuwa Mhandisi wa madaraja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ni Daraja laTanzanite, Kijazi Interchange na Mfugale Flyover.

Mhandisi Mfugale ndiye aliyebuni daraja la Malagarasi lenye urefu wa mita 178 kwa muda wa miezi mitatu na kuwa sehemu ya usanifu wa Daraja la Nyerere linalounganisha sehemu ya kati ya jiji na Kigamboni ambalo ni kwanza kujengwa baharini nchini lenye urefu wa mita 680 na upana wa mita 32.

Tangu alipoanza kazi kama fundi sanifu mwaka 1977 ufanisi wake ulimpandisha vyeo mbalimbali katika utumishi wake, ambapo aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Barabara za Mikoa mwaka 1992.

Baadaye aliteuliwa kuwa Mhandisi Mkuu wa madaraja, mwaka 1992 na akiwa masomoni Uingereza mwaka 1995 alitafiti na kutengeneza mfumo wa usimamizi wa madaraja nchini.

Pamoja na kuanza kazi mapema, Mfugale alisajiliwa kama mhandisi mtaalamu mwaka 1991, mhandisi mshauri mwaka 2014 na pia ni mwanachama wa Chama cha Wahandisi Tanzania.

Kutokana na utendaji wake, Mhandisi Mfugale alitunukiwa tuzo mbalimbali ambapo mwaka 2003 alipokea tuzo ya mafanikio katika fani ya uhandisi na tuzo ya mhandisi bora mwaka 2018

Aidha, Mhandisi Mfugale amekua Mwenyekiti wa Kikosi cha Wataalamu cha Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), ujenzi wa Dodoma Sports Complex na aliwahi kuwa mjumbe wa timu ya majadiliano ya mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge.

Wafanyakazi wenzake wamlilia

Hijja Malamla ni Mkurugenzi wa Fedha wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), aliyekuwa miongoni mwa wafanyakazi wenza wa Mhandisi Mfugale, anasema mbali na kuwa bosi lakini kiongozi huyo alisimama kama mzazi kwa wafanyakazi wenzake.

Anasema katika kipindi chote alichofanya kazi naye, alikuwa mithiri ya mzazi ambaye wakati wote alijikuta kushauri panapo kasoro.

Kwa mujibu wa Hijja, Mhandisi Mfugale katika uongozi wake TANROADS alipenda kutoa ujuzi na uzoefu wake hasa kwa wahandisi vijana.

“Alipenda ujuzi alionao uwafikie na wenzake, hakuwa mchoyo kimsingi alikuwa mlezi mzuri wa taaluma za vijana,” anasisitiza.

Hijja anaongeza kuwa Mhandisi Mfugale katika kipindi chote alichofanya kazi naye, hakuwahi kumuona akihamaki, badala yake alishauri na kusikiliza zaidi kisha kutoa maamuzi.

Anataja jambo lingine kumuhusu Mhandisi Mfugale ni kwamba hakuwa na haraka ya kufanya jambo ambalo aliona linahitaji utulivu.

Anamuelezea kuwa, alikuwa msikivu na hakudharau ushauri wa yeyote mwenye cheo na hadhi yoyote ofisini, bali akipenda kutoa changamoto kisha kutoa suluhu ya busara.

Anaeleza kuwa kiongozi huyo, alikuwa na maamuzi shirikishi kwani kila jambo bila kujali kubwa ama dogo aliishirikisha menejimenti kufanya maamuzi ya pamoja.

“Pamoja na yote Mzee Mfugale hakuwa na majivuno, hata ukimuona utadhani sio yeye mwenye jina kubwa linalofahamika na watu wengi,” anasema.

Anabainisha kuwa hata wakati watendaji wenye hadhi kama yake waliopatiwa walinzi binafsi, Mhandisi Mfugale alikataa hilo, kwa kile alichosema kuwa mlinzi wake ni Mungu pekee.

“Sikumuona akisema kwa hasira au jazba aliishia kushauri, huyu Mzee alikuwa na busara ya aina yake, hakika tumempoteza mtu makini,” anasema.

Anaeleza kuwa ukaribu wake na wafanyakazi haukuishia kazini pekee, bali hata aliwaalika mara kadhaa nyumbani kwake kwa shughuli za familia.

“Wema wake ulimfanya kuniunganisha familia ya TANROADS na familia yake, kama unavyofahamu wafanyakazi wengi inakuwa ngumu kupajua kwa mwenzako lakini Mzee wetu alitualika mara kwa mara,” Anaeleza.

Kuhusu mambo aliyochukizwa nayo, anayataja kuwa Mhandisi Mfugale, hakupenda uvivu, uzembe na kukosa udilifu katika kazi.

Anasema wakati wote alikuwa akiwaambia pengine kuna vitu vingi vinawashawishi TANROADS lakini ni vyema wafanye kazi kwa uadilifu, utendaji wao utaonekana tu.

Anafafanua kuwa pamoja na uzee wake lakini katika kazi iliyopangwa kumalizwa alikuwa tayari kutumia hata saa 24 ilimradi ikamilike, hivyo alikuwa mchapakazi mzuri.

Anaeleza kuwa, kiongozi huyo alipenda utani na watu wote, hilo aliahuhudiwa akilifanya mara kadhaa kwa watumishi wa ngazi mbalimbali wa TANROADS.

Wananchi

Hamza Kanali mkazi wa Dar es Salaam anasema alimtambua Mhandisi Mfugale baada ya uzinduzi wa Daraja la Mfugale Tazara jijini humo.

Anasema siku ya uzinduzi aliyekuwa Rais wakati huo alieleza sababu za kutoa jina hilo kwa Daraja lile, hivyo kupitia hilo alimfahamu.

Anafafanua kuwa kwa namna alivyoelezewa, anastahili kila aina ya heshima sio tu kwa utumishi wake, bali msaada alioutoa kwa wananchi kupitia maono yake.

Anaongeza pamoja na kwamba kila alilolifanya lilipata uwezeshaji kutoka serikalini lakini, taaluma yake amezitumia vyema kutekeleza wajibu wake na hatimaye imekuwa msaada kwa jamii.

“Siku hizi tunapita pale TAZARA bila msongamano kama ilivyokuwa awali, hata Ubungo pia, bila shaka kiongozi huyu ni miongoni mwa walioshiriki kufanikisha miradi hii,” anasema.

Changamoto

Akihutubia wananchi katika uzinduzi wa Barabara za juu za Mfugale aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dk. John Magufuli, alisema Mfugale amepitia changamoto nyingi katika utumishi wake ikiwamo kuamka nje ya nyumba aliyokuwa amelala na wakandarasi mkoani Ruvuma.

“Mfugale akiwa Songea kwa watani zangu wakiwa wamejenga kambi Matomondo na Kimesela, jioni yake walilala katika hako kajumba kesho yake waliamka saa nne wapo nje,” alisema.

Alieleza katika ujenzi wa barabara Matomondo fremu za greda ziliwahi kukatika wakati wa shughuli za utengenezaji wa barabara.

Aliongeza kazi hiyo iliendelea baada ya marehemu mzee Gama kuwaomba wanakijiji wa eneo hilo kuruhusu muendelezo wa utengenezwaji wa barabara hiyo kwa kuwa ilikuwa na manufaa kwao.

Hayati Dk. Magufuli alisema Mhandisi Mfugale amewahi kukaa ofisini bila kulala kwa siku tatu akibuni daraja la Umoja na kusahaulika katika utambulisho wa ufunguzi wa daraja hilo.

Hata hivyo, alimtaja kama mchapakazi, mzalendo, mbunifu na mwaminifu katika kazi zake na kwamba hakupendelewa kwa uamuzi wa flyover hiyo kupewa jina lake.

“Kwa naamna ya pekee nimpongeze mtendaji mkuu wa Tanroad Mhandisi Patric Mfugale kwa kusiriki kubuni nakusimamia michoro katika kutelekeza mradio huu,” alisema.

Maisha yake

Mhandisi Mfugale alizaliwa Desemba mosi, mwaka 1953, Ifunda mkoani Iringa na alianza elimu ya msingi mkoani humo.

Elimu yake ya Sekondari alihitimu mwaka 1975 katika Shule ya Sekondari Moshi.

Mwaka 1983, alihitimu Shahada ya kwanza ya uhandisi kutoka Chuo Kikuu cha Rokii India na shahada ya pili kutoka Chuo Kikuu cha Loughborough Uingereza mwaka 1995

Mwili wa Mhandisi Mfugale utasafirishwa kesho jioni kwenda Ifunda mkoani Iringa, kwa ajili ya maziko yatakayofanyika jumatatu.

Na JUMA ISSIHAKA

 

admin

admin

Stay Connected test

  • 139 Follower
  • 204k Subscriber
  • 23.9k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

August 7, 2023
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • Afya Makala
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Sports
  • Uncategorized

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In