Tuesday, May 20, 2025
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English English Kiswahili Kiswahili
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • English English
  • Kiswahili Kiswahili
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result
Mwanzo MAKALA

WANAWAKE WASIMULIA BIASHARA YA BARAKOA ILIVYOIMARISHA NDOA

admin by admin
September 10, 2021
in MAKALA
0 0
0
WANAWAKE WASIMULIA BIASHARA YA BARAKOA ILIVYOIMARISHA NDOA
0
SHARES
144
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

WIMBI la tatu la ugonjwa wa virusi vya corona (uviko-19) linaloikabili dunia, imegeuka kuwa fursa kwa idadi kubwa ya wanawake wengi nchini.

Hatua inatokana na kundi hilo kujikita katika biashara ya bidhaa mbalimbali zinazotumiwa katika afua ya kukabiliana na ugonjwa huo ikiwemo barakoa.

Wakizungumza Dar es Salaam, baadhi ya wanawake wanasema fursa wanayoitumia wakati wa ugonjwa huo, imewaokoa katika wimbi la manyanyaso kutoka kwa wenza wao, na kuwawezesha kumudu maisha ya familia na kujenga heshima.

Katika mazungumzo yao na UhuruOnline, wanawake hao wanasema biashara ya bidhaa za kujikinga na uviko-19, imekuwa mkombozi wa kile walichokiita dharau, kebehi na mateso dhidi ya wenza wao, huku baadhi yao wakikiri kunusurika kuachika katika ndoa zao.

Baadhi yao wanasema awali, wenza wao walikuwa wakiwaona ni mzigo ndani ya nyumba kwa kile walichoamini hawakuwa na mchango katika ustawi wa uchumi hasa linapokuja suala la matumizi ya chakula, kusomesha watoto na mambo mengine ya msingi ya kifamilia.

Shukurani Msemo ni mfanyabiashara wa barakoa katika kituo cha mabasi yaendayo Haraka (DART) cha Tiptop-Manzase, anasema biashara hiyo imemwezesha kuhudumia familia yake yenye mume na watoto watatu.

Shukurani anasema kabla ya biashara ya barakoa, aliishi maisha ya shida na mumewe ambaye, alikuwa akimuachia sh. 2,000 kwa siku kwa matumizi ya nyumbani, fedha ambayo haikutosha hata kwa mlo mmoja wa siku.

Anasema fedha alizokuwa akiachiwa kilitokana na uhalisia wa kipato cha mumewe kwa kuwa katika shughuli zake alizokuwa akifanya asingeweza kumwachia zaidi ya kiasi hicho.

“Wakati huo mimi sikuwa na shughuli ya kufanya, mume wangu ndiye aliyekuwa anakwenda katika mihangaiko ya kila siku lakini kipato chake hakikutosheleza huduma za familia hii yenye watu watano, nilijaribu kumwambia anisaidie mtaji nitafute biashara lakini ilishindikana,” anasema.

Shukurani anasema alipata wazo la kuuza barakoa, lakini hakuwa na mtaji, hivyo ilimlazimu kuweka akiba ya sh. 500 kila siku kati  ya sh. 2,000 alizokuwa akiachiwa kwa matumizi ya chakula ya nyumbani. Hivyo alitumia sh. 1,500 kila siku pasipo mumewe kujua.

Mjasiriamali huyo anasema kuwa baada ya kuhifadhi kiasi hicho cha fedha alifikisha sh. 10,000 zilizotosha kununua boksi moja la barakoa na kuanza biashara hiyo.

“Kuna rafiki yangu alinishauri kuhusu biashara ya barakoa, wakati huo yeye alikuwa anafanya biashara hiyo, ndipo nilipopata wazo la kuhifadhi fedha na baada ya mwezi mmoja ilifika sh. 10,000 akanipeleka kununua boksi moja na nikaanza biashara,” anasema.

Shukurani anasema baada ya kuanza biashara hiyo, wamekuwa wakipata milo mitatu kwa siku na yeye akiwa ni tegemeo kubwa ndani ya familia.

“Kuna wakati mume wangu haniachii fedha za matumizi ya siku, lakini anakuta nimepika na wanangu wanakula vizuri, wote tuna furaha. Kabla ya biashara hii alikuwa akiniita majina yasiyofaa lakini sasa naona upendo na heshima imeongezeka,”anasema.

Shukurani anadokeza kwa siku anapata kati ya sh. 15,000 hadi 20,000 kulingana na biashara kwa siku husika na amejipanga kuanzisha biashara nyingine ili kuongeza kipato katika familia.

Kauli ya Shukurani inaungwa mkono na Naima Sauli, anayefanya biashara ya barakoa jijini, ambaye anasema huangalia fursa ya maeneo yenye mikusanyiko ya watu yanayolazimisha uvaaji wa barakoa akitoa mfano wa hospitali na maeneo mengine muhimu.

Anasema biashara ya barakoa anafanya zaidi katika Hospitali za Mnazi Mmoja, Muhimbili na Uwanja wa Benjamin Mkapa wakati matukio ya michezo.

“Kwa mfano siku ya Tamasha la Yanga nilikwenda na barakoa zangu nilizotengeneza kwa fundi nimeziweka nembo ya Yanga, nilirudi nyumbani na sh. 100,000 kila barakoa niliiuza sh. 2,000,” anasema.

Anasema biashara hiyo imemfanya kuona umuhimu wa kutumia fursa katika jambo lolote linalotokea duniani na anasisitiza bila barakoa asingepata mafanikio aliyonayo.

“Sina mume lakini nina watoto watatu, kabla nilifanya biashara ya mamalishe, lakini uuzaji wa barakoa una faida kuliko mamalishe, kwa sasa nimeamua kuacha na kujikita katika barakoa,” anasema.

Anasema kupitia biashara ya barakoa, anamudu gharama za nauli ya wanawe kwenda na kurudi shuleni, kuihudumia familia, kulipa kodi ya nyumba mambo ambayo alipokuwa mamalishe alishindwa kuyatimiza kwa wakati.

“Nilipokuwa mamalishe kuna wakati nilibaki na nauli yangu, maana yake nikiwapa watoto waende shule mimi nabaki nyumbani au nikienda nayo mimi kazini watoto hawaendi shule, maisha yalikuwa magumu sana,” anasema.

Wakati Naima akitoa maelezo hayo, Lucy Koja, anayeuza barakoa katika soko la Mabibo, anasema ingawa biashara hiyo imedorora sokoni hapo kutokana na mwamko mdogo wa watu kuvaa barakoa, lakini imetofautisha maisha yake ya awali na sasa.

“Zamani nilikuwa nauza makopo nayaokota nakwenda kupima na kuuza, kwanza nilionekana chizi maana ile shughuli unatafsiriwa vibaya, pili niliishia kupata hela ya kula mlo mmoja wa siku. Lakini kwa sasa nimemfuata mwanangu kijijini naishi naye kuwa kuna nina uhakika wa kipato,” anasema.

Kwa upande wake, Nawale Singano anayefanya biashara katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), anasema barakoa zina historia kubwa katika maisha ya ndoa.

Anasema kabla ya kuanza biashara hiyo alinusurika kuachika, kwani ulifika wakati mumewe alikosa fedha za kuhudumia familia na kumtaka arudi kwa wazazi wake mkoani Songwe.

Nawale anasema mumewe alifikia uamuzi huo kwa kile alichodai kuwa asingeweza kuihudumia familia kutokana na kipato kidogo, hivyo alitaka abaki mwenyewe.

“Kila biashara niliyofikiria kufanya kumsaidia mume wangu mtaji wake ulianzia sh. 100,000 na zaidi, hivyo sikuwa na uwezo wa kupata, lakini nilipoona wanawake wengine barabarani wanauza barakoa niliuliza nikaambiwa boksi moja ni sh. 10,000 nilitafuta nilipopata nikaanza biashara na sasa mambo mazuri

“Mwenzangu akitoka nami nikitoka tukirudi tunakusanya kiasi kikubwa, hivi ninavyokwambia tuna akiba tunataka kufungua duka la bidhaa mbalimbali, uviko-19 imekuja na fursa kubwa hasa kwetu wanawake.

“Tulikuwa tukigombana na mume wangu kila siku akinitaka nirudi nyumbani, lakini siku hizi upendo umeongezeka, tunazungumza vizuri na mipango yetu ni mizuri, nawashauri wanawake watumie fursa zilizoko kujipatia kipato,” anasema Nawale.

JUMA ISSIHAKA NA IBRAHIM HUSSEIN (UDSM)

admin

admin

Stay Connected test

  • 139 Follower
  • 204k Subscriber
  • 23.9k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

August 7, 2023
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • Afya Makala
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Sports
  • Uncategorized

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In