Tuesday, May 20, 2025
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English English Kiswahili Kiswahili
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • English English
  • Kiswahili Kiswahili
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result
Mwanzo MAKALA

LATIFA ‘HOUSE GIRL’ WA ZAMANI ANAYESIMULIA UKATILI WA KINGONO KUTOKA KWA MWAJIRI

28>> Umri wa Latifa aliyekuwa mfanyakazi wa ndani, anasimulia ukatili wa kingono

admin by admin
October 12, 2021
in MAKALA
0 0
0
LATIFA ‘HOUSE GIRL’ WA ZAMANI ANAYESIMULIA UKATILI WA KINGONO KUTOKA KWA MWAJIRI

Latifa Salumu

0
SHARES
171
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

WASICHANA wa kazi za ndani maarufu kama ‘House Girl’ ni moja ya makundi muhimu katika jamii kutokana na majukumu makubwa wanayoyafanya.

Wamekuwa msaada mkubwa katika kutunza nyumba na kulea familia za waajiri wao.

Hata hivyo, wamekuwa wakikumbana na changamoto nyingi katika jamii inayowazunguka, baadhi yao hupata mikasa tofauti kutokana na kile kinachodaiwa kuwa manyanyaso kutoka kwa baadhi ya waajiri wasiojali umuhimu wao.

Umasikini na kushindwa kuendelea na masomo, kumetajwa ni mojawapo ya vyanzo vya wasichana hao kwenda katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma na Arusha kwa lengo la kufanya kazi hizo za ndani ili wapate vipato vya kuhudumia familia zao.

“Nimeteseka, nilitolewa nyumbani kwetu nikaambiwa nakuja mjini kusoma ‘tuition’, lakini mambo yakawa tofauti.

“Nilipelekwa kufanya kazi za ndani, nilipitia mateso mengi ikiwa ni pamoja na kutolipwa mshahara na kulazimishwa kushiriki ngono.”

Hivi ndivyo anavyosimulia Latifa Salumu, binti wa miaka 28 aliyepitia mikasa ya kunyanyaswa kijinsia, kufanyiwa ukatili wa kingono wakati akiwa na miaka 17 akifanya kazi kwa mwajiri wake wa kiume.

Latifa anasema mazingira ya kufanya kazi za ndani huwa shubiri unapokutana na mwajiri ambaye hana utu, upendo na hofu ya Mwenyezi Mungu katika kumjali binti wa kazi, baadhi yao huwaona hawana thamani kama walivyo watoto wao.

AFUNGUKA ALIVYOKABILIWA NA UKATILI WA KINGONO

Latifa, anasema baada ya kuajiriwa katika nyumba hiyo akiwa na miaka 17, mama mwenye nyumba, alikuwa anamwachia kufanya majukumu yote ya kutunza familia kwani hakuwa na muda wa kukaa nyumbani na familia yake.

LATIFA aliyejitanda ushungi akitoa elimu kwa mabinti katika eneo la Chanika Jijini Dar es Salaam

“Mama ambaye ni mwajiri wangu, alikuwa ‘bize’ sana, akitoka nyumbani saa 11 alfajiri, anarudi usiku  ilinilazimu mimi ndiye niwe mlezi wa mtoto wake mdogo,” anasema.

Mwanadada huyo anaeleza kuwa, alianza kukabiliwa na  vishawishi vya mume wa mwajiri wake, alitafuta mwanya wa kuzungumza na mama huyo, lakini alikuwa hampi nafasi kutokana na kila alipomuomba kuzungumza naye, alijibiwa hana nafasi.

Anasema kitendo cha kutolipwa mshahara kwa kipindi cha miezi minane, kilimfanya aingie katika vishawishi na mitego ya baba mwenye nyumba ambaye alimfanyia vitendo vya ukatili wa kingono.

Wakati mama mwenye nyumba alipokuwa anaondoka nyumbani alfajiri, Latifa anasema alikuwa anamwambia akamchukue mtoto chumbani kwake ambako analala na mumewe.

Latifa anaeleza kwamba, alikuwa analazimika kila siku alfajiri kwenda kumgongea mume wa mama huyo ili kumchukua mtoto aanze kumuhudumia.

Kitendo cha kutekeleza maagizo ya mwajiri wake cha kumfuata mtoto kila siku chumbani, kiliibua changamoto na kutoa mwanya kwa mume wa mama huyo kuanza kumrubuni, hatimaye alifanyiwa ukatili wa kingono.

Latifa anasema baada ya kufanyiwa kitendo cha ukatili wa kingono, mama mwenye nyumba, aligundua ukatili aliofanyiwa na mumewe, hivyo alimfukuza katika nyumba hiyo bila kulipwa chochote.

“Niliondoka katika nyumba ile bila kulipwa fedha yoyote, kwanza nilikuwa nafanyakazi bila mkataba, maisha yangu yalikuwa magumu,” anasema Latifa.

Hata hivyo, Latifa anasema baada ya kuondoka katika familia hiyo, alipata kazi ya kufanya miamala ya simu, kazi ambayo hakudumu muda mrefu kwani hakuwa akilipwa ujira kwa wakati.

KUHUSU KIKUNDI CHA SAUTI YA JAMII

Latifa anasema kuwa, mwaka 2020 alibahatika kuhudhururia semina iliyohusu namna wasichana wa kazi za ndani kutambua haki zao, iliyoandaliwa na Taasisi ya Sauti ya Jamii iliyopo Kipunguni, Dar es Salaam.

Kupitia semina hiyo, Latifa alijifunza mambo mbalimbali zikiwemo haki za wasichana wa kazi za ndani kujua wajibu na haki zao za msingi.

ALIVYOANZA HARAKATI

Kupitia semina hiyo, Latifa anasema alipopata elimu na kujitambua thamani yake, aliamua kuanza kutafuta wasichana wa kazi za ndani kwa kupita nyumba moja hadi nyingine kuomba kuzungumza nao ili awape elimu.

Agosti mwaka huu, alianza harakati hizo maeneo ya Chanika, Dar es Salaam kupitia wajumbe wa nyumba 10 kutambua nyumba zenye wasichana walioajiriwa kufanya kazi za ndani, alianza na wasichna 20.

Anasema amekuwa akiwafundisha wasichana hao wa kazi za ndani kufahamu haki zao, kuhakikisha wanajua haki zao zikiwemo kuwa na mikataba ya ajira kutoka kwa waajiri wao.

MAFANIKIO YAKE

Latifa anasema tangu aanze kutoa elimu hiyo, amefanikiwa kutoa elimu hiyo kwa wasichana 40 na waajiri 30, anashukuru mwitikio umekuwa mkubwa na kuanzisha kikundi ambacho wanatoa elimu sehemu mbalimbali.

Kupitia mafunzo hayo, amefanikiwa kuwaeleza wanaowaajiri wasichana wa kazi za ndani, kutambua umuhimu wa mwanamke kukaa na kuzungumza wasichana hao, badala ya kuwatenga kwani hufanya hivyo kutasaidia kutatua changamoto mbalimbali.

Aidha, anasema katika mafundisho anayoyatoa, amekutana na wasichana 30 wanapitia changamoto mbalimbali kama ubaguzi, unyanyasaji na kutolipwa mishahara yao kwa wakati.

CHANGAMOTO

Latifa anasema changamoto anayokutana nayo ni baadhi ya waajiri wasivyokuwa na utu, kujenga chuki dhidi yake kutokana na elimu anayotoa kwa wasichana hao.

Changamoto zingine ni baadhi ya mabinti wanaopata elimu nyumbani kwake, kutokurudi kwa waajiri wao kutokana na waajiri kuwazuia kufanya hivyo.

MATARAJIO YAKE

Latifa anatamani kuwafikia wasichana wengi katika mikoa mbalimbali nchini ili watambue haki zao za msingi na namna bora ya kukabiliana na rushwa ya ngono na ukatili.

Anaomba ushirikiano kutoka kwa serikali na taasisi mbalimbali, zimwezeshe kuwafikia wasichana wengi zaidi wanaofanyiwa vitendo vya ukatili na waajiri wao.

WITO WAKE

Latifa anatoa ushauri kwa wasichana wa kazi za ndani kutokukubali kushawishiwa kufanyiwa ukatili wa kingono, badala yake, wanapoona mazingira yasiyofaa, watoe taarifa kwa mamlaka husika.

HISTORIA YAKE

Latifa ni binti mwenye umri wa miaka miaka 28 mzaliwa Shinyanga, alilelewa na mzazi mmoja kutokana na mama yake mzazi kupoteza maisha, akiachwa akiwa na umri wa mwaka mmoja.

Kutokana na mama yake mzazi kufariki dunia, baba yake alihamisha makazi kutoka Shinyanga kwenda Dar es  Salaam, alianza elimu ya msingi mwaka 2000 katika Shule ya Msingi  Kisanga, Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.

Mwaka 2007 alianza elimu ya Sekondari katika Shule ya Mwanalumango, hukohuko Kisarawe na kuhitimu kidato cha nne mwaka 2010, baadaye alianza kufanya kazi za ndani.

Na IRENE MWASOMOLA          

admin

admin

Stay Connected test

  • 139 Follower
  • 204k Subscriber
  • 23.9k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

August 7, 2023
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • Afya Makala
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Sports
  • Uncategorized

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In