Saturday, July 4, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

WARIOBA ANG’AKA

>> Ataka wabaguzi wakemewe, hawana nia njema na nchi

admin by admin
October 13, 2021
in Habari Kitaifa
0
WARIOBA ANG’AKA

WAZIRI Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, akizungumza katika Kongamano la Kumbukizi ya Miaka 22 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Kigamboni, Dar es Salaam. (Picha na Jumanne Gude).

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, ameng’aka na kusema jamii ya Watanzania, inapaswa kuwakemea kwa nguvu zote wanaotaka kuleta ubaguzi miongoni mwao kwa sababu hawana nia njema na Tanzania.

Jaji Warioba amesema udini, ukabila, ukanda, uvyama katika kipindi cha hivi karibuni, vimeonekana kuzungumzwa kwa kiwango kikubwa, hali inayoweza kuhatarisha misingi ya amani ya taifa iliyoasisiwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Aliyasema hayo Dar es Salaam, kama sehemu ya hotuba yake wakati akifungua Kongamano la Kumbukizi ya miaka 22 ya kifo cha Hayati Mwalimu Julius Nyerere, lililofanyika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

“Viongozi tukemee wanaotaka kuleta hayo (Ya kibaguzi), Watanzania tuwe kitu kimoja, tufanye mambo yetu, kuijenga nchi yetu,” alisema.

Kauli yake, imekuja siku chache baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, akemee ubaguzi unaoonekana kuzungumzwa na baadhi ya watu, wakiwemo viongozi hasa linapokuja suala la uwajibishwaji katika utumishi wa umma.

Waziri mkuu huyo mstaafu alisema amani imejengwa kwa jasho na kwamba, haikupatikana kwa mara moja, hivyo jamii isiruhusu kuchezewa kwa tunu hiyo ambayo imeendelea kuwepo nchini kwa kipindi kirefu.

“Juzi Rais (Samia), aliongea mambo haya, kukemea udini, ukabila, ukanda na uvyama, nilimhurumia hii ni misingi ya umoja wetu, ambayo imeanza kuchezewa.

“Amani haikuja hivihivi, ilijengwa pamoja na umoja na hizi ni moja ya kazi za mwanzo kabisa alizozifanya Mwalimu wakati wa uongozi wake kwa taifa hili.

“Mwalimu alitaka kuondoa ukabila na aliishi hivyo, marafiki zake wa karibu, ukimzungumzia Mzee Kawawa, alikuwa ni muislamu, yeye alikuwa mkristo, mkatoliki,” alisema.

Kadhalika, alisema uadilifu wa Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake haukuwa na shaka, kwamba hata maadui zake walidiriki kukiri juu ya sifa hiyo ya Mwalimu.

Alisema Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake aliishi maisha ya kawaida, yasiyo na mbwembwe na alithamini utu na haki kwa wote.

Jaji Warioba ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati wa utawala wa Nyerere, alisema wakati taifa linakumbuka miaka 22 ya kifo chake, linapaswa kuishi matendo yake badala ya yanayoandikwa kumhusu.

“Ninatamani sote tufahamu kuwa maisha yake aliyoyaishi ni muhimu tukajifunza kuyahusu kuliko kumbukumbu za kifo chake,” alisema.

Alisema Mwalimu pamoja na kuwa mtoto wa chifu na nafasi kubwa aliyopewa katika jamii, bado alibaki mtu wa kawaida mwenye mawazo na mwelekeo wa mtu wa kawaida.

Jaji Warioba alisema Mwalimu alikuwa na imani ya utu wa binadamu, aliamini watu wote ni sawa kwamba kila mtu anastahili heshima.

“Mwalimu alipochaguliwa kuwa Rais, wakati ule ilikuwa ni kawaida watu kumuita mtukufu Rais, lakini yeye alikataa kuitwa mtukufu Rais, akasema yeye si mtukufu, mtukufu ni Mungu, yeye ni binadamu na mwalimu wa kawaida. Ndio chanzo cha kumuita Mwalimu,” alisema Jaji Warioba.

Pia, alisema mkewe Maria Nyerere, ilikuwa kawaida wakimuita ‘First Lady’, lakini alikataa na kusema huyu ni Mama Maria, ndio jina hilo limekua kama cheo.

Jaji Warioba alisema Mwalimu alikataa jina lake kutumiwa kwa mambo mbalimbali, kama majina ya barabara, majengo na kwamba, alipokuwa Rais hakukuwa na barabara iliyokuwa na jina lake.

Alisema Mwalimu hakupenda viongozi kuitwa mheshimiwa, aliamini Watanzania wote ni ndugu na alitaka waitane ndugu ikiwamo yeye kuitwa ndugu Rais.

“Wakati wake, kumuita ndugu Rais ilikuwa jambo la kawaida. Uhusiano wake ni kweli alikuwa anafanya kazi na viongozi, lakini hakusahau marafiki zake wa kawaida na alikuwa anakutana nao na wazee wanacheza bao pale Msasani na kunakuwa na utani mwingi.

Jaji Warioba alisema Mwalimu Nyerere alikuwa anaamini haki kwa wote, hata katika maandiko yake alikuwa anasisitiza haki na ndiyo ulikuwa msingi kwenye mapambano ya kujikomboa kutoka kwa wakoloni.

Alisema Tanzania ina zaidi ya makabila 120, lakini Mwalimu Nyerere alitumia lugha ya Kiswahili kuyaunganisha makabila yote kwa kujenga, umoja, mshikamo na hadi sasa nchi ina amani.

“Ili kuheshimu hili, ufike wakati elimu yetu yote iwe kwa lugha ya Kiswahili,” alisema Jaji Warioba.

Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere (Mwalimu Nyerere Foundation), Joseph Butiku, akizungumza katika kongamano hilo, alikemea mmomonyoko wa maadili kwa viongozi wa umma, ili kuendelea kulinda mafundisho ya Mwalimu Nyerere.

“Ukiwa na nafasi ya uongozi, unatakiwa utambue ile ni dhamana, uongozi ni dhamana, kwamba vitu ulivyopewa uvisimamie si vyako, ni vya wote.

“Weka utaratibu wa kuvitumia kwa faida ya watu wote sio kwa ajili ya mtu fulani au kikundi cha watu fulani na wengine unawasahau,” alisema.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Stephen Wasira, akichangia mada za kongamano hilo, alisema chuo hicho kimekuwa na utamaduni wa kuandaa makongamano hayo mara tatu kwa kila mwaka kwa Tanzania Bara na Visiwani.

Akimzungumzia Mwalimu Nyerere, alisema katika uzoefu wake wa kisiasa, hamfahamu kiongozi mwingine wa kumlinganisha na Mwalimu Nyerere kimaadili.

“Alikuwa wa kawaida kabla ya uongozi, akiwa uongozini na hata baaa ya uongozi, hakuwaibia wananchi,” alisema Wasira.

Kongamano hilo lililoongozwa na Mada kuu: ‘Maono ya Mwalimu Nyerere katika uongozi, maadili, umoja na amani kwa maendeleo ya jamii’ lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa, kisiasa, wananchi na wanataaluma.

Na WILLIAM SHECHAMBO

Previous Post

MSD YAFANYA KUFURU USAMBAZAJI DAWA NCHINI

Next Post

MPANGO ATOA MAAGIZO BWAWA LA JULIUS NYERERE

admin

admin

Next Post
MPANGO ATOA MAAGIZO BWAWA LA JULIUS NYERERE

MPANGO ATOA MAAGIZO BWAWA LA JULIUS NYERERE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved