Tuesday, March 10, 2026
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English English Kiswahili Kiswahili
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • English English
  • Kiswahili Kiswahili
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result
Mwanzo Habari Kitaifa

RAIS SAMIA AKONGA NYOYO ZA WASOMI

>>> Ni KUELEKEA mwaka mmoja akiwa madarakani

admin by admin
February 26, 2022
in Habari Kitaifa
0 0
0
RAIS SAMIA AKONGA NYOYO ZA WASOMI

RAIS Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
148
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

MWANASIASA nguli nchini, Balozi Amina Ali, ameutaja mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani, kuwa nchi imefunguka kwa mafanikio.

Mwanasiasa huyo aliyeshika nafasi ya pili katika mchujo wa ndani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika kuwania urais mwaka 2015, amesema Rais Samia amelifanya taifa kuwa na nguvu na kuthaminika duniani kutokana na kufungua milango ya kidiplomasia na kiuchumi.

Balozi huyo wa zamani wa Umoja wa Afrika, amewataka wananchi kudharau wanasiasa uchwara wanaotafuta hila, kwa sababu ukweli unaonekana kuwa mwaka mmoja wa uongozi ametosha katika nafasi ya mrithi wake Hayati Dk. John Magufuli baada ya kuendeleza miradi ya kimkakati.

Amesisitiza kuwa Rais Samia amefiti na ni jahazi lisiloyumbishwa na mawimbi, kwa kuwa amesimama kidete katika kuhakikisha maendeleo ya sekta madini, afya, elimu, uchumi, siasa na jinsia yanafikiwa ipasavyo.

DIPLOMASIA

Akizungumza katika mahojiano maalumu, Balozi Amina amesema, katika kipindi hicho Rais Samia amefanya vizuri katika kila sekta na kuifungua nchi katika diplomasia hatua iliyolijengea heshima taifa.

“Kuanzia alivyounda Wizara ya Mambo ya Nje tuliona mwelekeo wake katika kuijenga Tanzania yenye nguvu na kuipandisha hadhi ndani ya Afrika Mashariki, Kusini mwa Bara la Afrika na duniani kwa ujumla,” alisema.

Amesema Rais Samia amerejesha idara zote muhimu katika wizara hiyo, ikiwemo ya diplomsia na uchumi ambayo mkurugenzi wake alikuwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Balozi Edwin Rutageruka, aliyefariki hivi karibuni.

Alisema utendaji wake umefunguka na kumgusa kila mtu hatua iliyoweka picha ulimwenguni kuwa Rais mwanamke wa mfano, anayewafanya Watanzania kutembea kifua mbele.

“Sisi mabalozi ni mashuhuda wa hilo, hatuoni haya kujitambulisha kwa wenzatu huko duniani kuwa tunatoka Tanzania inayoongozwa na Rais Samia,”alisema.

Balozi Amina alisisitiza kuwa Rais Samia amemaliza kiu ya wengi katika masuala ya diplomasia na uchumi shirikishi.

UCHUMI

Akizungumzia maendeleo ya kiuchumi alisema uongozi wa  Rais Samia umeonyesha mwelekeo wa sekta hiyo na kufungua uchumi wa nchi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

“Makusanyo yameongezeka kwa kuwa Tanzania ina utulivu wa maamuzi na umakini katika kusimamia uchumi ukweli tuna picha halisi ya Tanzania ijayo ya mbele ambayo ni ya uchumi si wa kufikirika ila unaoonekana kwa kila mtu,”alisema.

Alisema ni Rais anayejua tulipotoka, tulipo na tunapotakiwa kwenda hatua iliyomlazimu kuhakikisha miradi yote ya kimkakati hususani iliyoachwa na mtangulizi wake Hayati Dk. Magufuli anaiendeleza ikiwemo ujenzi wa miundombinu kama madaraja, barabara vitega uchumi muhimu kama Bwawa la Mwalimu Nyerere na Reli ya Kisasa

UWEKEZAJI

Mwanasiasa huyo alieleza kuwa sekta ya uwekezaji sasa imekua na wawekezaji wengi zaidi wamejitokeza.

Alisema safari zake za nje zimepunguza vikwazo, kuondoa kero zisizo za lazima na kusimamia ipasavyo utendaji kwa kudhibiti urasimu zimewavuta wawekezaji wengi kuja nchini.

“Sekta ya uwekezaji imekua inaonekana anawafuata wawekezaji huko huko nchini mwao, anafanaya nao mazungumza akiwa na timu ya wataalamu na wanaona fursa zilizopo wanakuja huyu ndiyo Rais Samia,”alisema.

BIASHARA

Alisema sekta ya biashara imekua na kufungua fursa za masoko ndani na nje ya nchi.

Balozi AMina alisisitiza kuwa kwa sasa bidhaa za Tanzania zina soko kubwa nje ya nchi ikiwemo la kahawa, mboga, viungo na rasirimali bahari wakiwemo dagaa ambao wana soko kubwa mjini Lumbumbashi nchini DRC Congo.

SIASA

“Mbali na hayo amekuwa ni kiongozi anayeonyesha kwa vitendo nidhamu ya hali ya juu kwa waasisi wetu na viongozi waliomtangulia kwa kusifu mazuri waliyofanya na kuayaendeleza,”alisema.

Alieleza kuwa mwaka mmoja wa Rais Samia amekijengea Chama  heshima ndani na nje ya nchi na hotuba yake katika ufunguzi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere juzi mkoani Pwani wilayani Kibaha, imejipapanua namna Chama kitakavyojikita katika kuwandaa viongozi walio na maadili, weledi na utumishi wenye nidhamu kwa kuwa na elimu ya Itikadi.

ELIMU

Alisema uongozi wa Rais Samia katika mwaka mmoja wa utendaji wake, umejionyesha alivyogusa sekta zote muhimu ikiwemo ya elimu ambapo ameendelea hatua ya elimu bure kuweka mazingira rafiki ya kusomea na kujali mahitaji ya walimu na watendaji wengine.

“Pia amefungua milango ya Watanzania kupata fursa ya masomo na kubadilishana uzoefu kutoka nchi nyingine duniani,”alisema.

JINSIA

Akizungumzia maendeleo sekta ya jinsia Balozi Amina alisema Rais Samia ni mwanamke wa pekee ambaye kama ni jahazi limetulia, kwakuwa ametambua thamani ya mwanamke bila wivu wala choyo amedhamiria kuwashika mkono na kuwainua.

Kwa upande wake mwanasiasa mkongwe nchini, Gertrude Mongella, alisema katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Rais Samia jambo la kujivunia ni kuendelea kuwepo kwa amani na utulivu nchini.

Alieleza mkuu huyo wa nchi ameiongoza nchi kufuata misingi iliyoasisiwa na waasisi wa taifa ndiyo sababu ya kuendelea kuwepo kwa amani na utulivu.

“Naomba niongee kwa sentensi moja kwamba, moja ya jambo tunalojivunia katika mwaka mmoja wa serikali hii ni kuendelea kuwepo kwa amani na utulivu na kazi inaendelea,” alieleza kwa ufupi.

Naye, mhadhiri wa zamani wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Dk. Ave Maria Semakafu, alisema Rais Samia ameandika historia katika kipindi hicho.

“Ameandika historia kwani ni mara ya kwanza tunapata kiongozi wa juu mwenye jinsia tofauti, Rais Samia amekuwa mwanamke wa kwanza kuwa rais hilo ni jambo kubwa kwetu,” alisema.

Alisema pia Watanzania wanapaswa kujivunia juhudi za kiongozi huyo za kuhakikisha anatekeleza haki na usawa katika fursa zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Alibainisha jambo jingine katika kipindi hicho ni kufanikisha kupatikana kwa Waziri wa Ulinzi wa kwanza mwanamke Dk. Stergomena Tax, jambo lililowashangaza wengi.

Dk. Semakafu ambaye pia ni mwanaharakati wa jinsia, alifafanua matendo ya Rais Samia katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wake yameendelea kuithibitishia jamii kwamba mwanamke anastahili haki zote kama ilivyo wanaume.

“Utaona kwa sasa tuna wanawake wengi katika Baraza la Mawaziri hii inatokana na hatua yake ya kuwapa fursa wanawake, tumeona katika teuzi nyingi anazozifanya anazingatia usawa wa jinsia,” aliongeza.

Dk. Semakafu ambaye ni Mratibu wa Jumuiya ya wanawake wenye itikadi tofauti za kisiasa (TWCP-Ulingo), alisisitiza mwaka mmoja wa uongozi wa Rais Samia umeonyesha dalili njema katika maridhiano ya kisiasa ambapo, aliagiza kuundwa tume ya kushughulikia changamoto zinazosababisha maelewano duni baina ya vyama vya siasa.

Aliongeza kwamba Rais Samia ameendelea kuonyesha uhalali wa mwanamke kupewa uongozi kwani wana sifa zote yaani uwezo na akili.

Alitaja jambo lingine la kujivunia ni uamuzi wake wa kuyaimarisha majukwaa ya wanawake aliyoyaasisi, akisema hayo yatawatoa wanawake kutoka kufanya biashara ndogondogo na kuwaingiza kushiriki katika uchumi wa viwanda.

Hatua hiyo inafikiwa ikiwa Rais Samia anatarajia kutimiza mwaka mmoja wa uongozi wake Ifikapo Machi 19 mwaka huu.

Aidha katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wake, Rais Samia ameonyesha mwelekeo wa siasa za urafiki, baada ya kukutana na viongozi wa vyama vya upinzani akiwemo Tundu Lissu.

Pia, katika kipindi hicho ameiingiza Tanzania katika ramani ya dunia kwa kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na mataifa mbalimbali, hivyo kuleta tija ya misaada na mikopo ya masharti nafuu.

Rais Samia ndani ya kipindi hicho amefanya ziara kadhaa katika mataifa mbalimbali likiwemo la Kenya na kusababisha kuondolewa kwa vikwazo vya kibiashara vilivyokuwepo baina ya mataifa hayo.

Pia, ziara yake ya kwenda Ulaya imerudisha uhusiano baina ya Umoja wa Ulaya (EU) na Tanzania na hivyo kuwezesha misaada iliyokuwa ikitolewa na jumuiya hiyo kuendelea kutolewa ukiwemo wa ujenzi wa viwanja vya ndege.

Katika uwajibikaji ndani ya serikali, Rais Samia ndani ya mwaka mmoja ameonyesha uwazi, uzalendo na uchungu na fedha za umma, hilo limejidhihirisha wakati wa matumizi ya fedha za mkopo kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuleta ustawi na kukabili Uviko-19.

Kuhusu usawa wa jinsia, Rais Samia amekuwa akilitekeleza hilo kwa kuzingatia jinsia zote katika teuzi alizozifanya na kuvunja rekodi ya baadhi ya nafasi kuwapa wanawake ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuasisiwa kwa Tanzania.

Mariam Mziwanda Na Juma Issihaka

admin

admin

Stay Connected test

  • 138 Follower
  • 205k Subscriber
  • 23.9k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

August 7, 2023
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0

The Founding of YouTube A Short History

March 9, 2026

İdman bahisində Mostbet platformasında fırıldaqçılığa qarşı nəzarəti gücləndirmək

March 9, 2026

Эффективная связь со службой поддержки 1xbet для решения проблем

March 9, 2026

Hur man hittar casinon med de mest generösa reload-bonusarna online

March 8, 2026

Recent News

The Founding of YouTube A Short History

March 9, 2026

İdman bahisində Mostbet platformasında fırıldaqçılığa qarşı nəzarəti gücləndirmək

March 9, 2026

Эффективная связь со службой поддержки 1xbet для решения проблем

March 9, 2026

Hur man hittar casinon med de mest generösa reload-bonusarna online

March 8, 2026
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • casino utan svensk licens
  • Forex News
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • News
  • Post
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Sports
  • Uncategorized

Recent News

The Founding of YouTube A Short History

March 9, 2026

İdman bahisində Mostbet platformasında fırıldaqçılığa qarşı nəzarəti gücləndirmək

March 9, 2026

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In