Tuesday, May 20, 2025
27 °c
Dar es Salaam
25 ° Thu
25 ° Fri
25 ° Sat
25 ° Sun
25 ° Mon
English English Kiswahili Kiswahili
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • English English
  • Kiswahili Kiswahili
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result
Mwanzo MAKALA

BURIANI RASHID ZAHOR ‘DOCTOR’

admin by admin
December 4, 2021
in MAKALA
0 0
0
BURIANI RASHID ZAHOR ‘DOCTOR’

MAREHEMU Rashid Mohammed Zahor

0
SHARES
145
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

ILIKUWA saa 4:31 asubuhi ya jana wakati nikiingia ofisini nilipokea simu kutoka kwa mmoja wa waandishi wa habari wa gazeti hili Uhuru, William Shechambo, nikajua anataka kunijulisha hali za wagonjwa wake, maana alikuwa anauguliwa na mkewe na mwanawe.

Kama nilivyohisi kweli alinielezea juu ya hali za wagonjwa wake, huku akiniambia kwamba wanaendelea vizuri na anamshukuru Mungu kwa jinsi wanavyoendelea kuimarika. Basi nami nikamueleza kwamba hayo ndiyo majukumu ya mume kwa mke na mzazi kwa mtoto kwamba lazima uwajibike katika kila changamoto wanazozipitia.

Basi baada ya maelezo yangu kwake, Shechambo alinieleza:”Chief hata hivyo nimepokea taarifa za kustusha kutoka kwa ndugu yake na Zahor, kwamba amefariki dunia,” alisema Shechambo na kufafanua kwamba aliyempigia simu alijitambulisha anaitwa Zahor na ni ndugu wa Rashid Zahor ambaye sasa ni marehemu.

Kwa mujibu wa Shechambo mtoa taarifa (Zahor) alimweleza kwamba aliipata namba yake baada ya kupekua simu ya marehemu na kugundua ndiye mtu aliyekuwa akiwasiliana naye sana kupitia ujumbe mfupi wa maandishi na ndipo alipoamua kumpigia na kumpa taarifa za kifo cha nduguye huyo.

Shechambo alisema Zahor (mtoa taarifa), alimweleza kwamba nduguye (Rashid) alifariki dunia saa tatu asubuhi huko Chanika, nyumbani kwa dada yake kutokana na maradhi ya kisukari na shinikizo la damu, ambayo yamekuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.

Nilistuka na kuingiwa na simanzi kubwa kutokana na ukweli kwamba si muda mrefu niliwasiliana na Zahor, huku akinielezea changamoto za kiafya anazopitia.

Alinieleza jinsi anavyopambana na kisukari na vidonda vya tumbo, nami nikamsisitizia umuhimu wa kuzingatia tiba na masharti ya madaktari.

Hata hivyo, hivi karibuni nilimpigia simu kumjulia hali, lakini simu yake iliita bila kupokelewa, nikatuma ujumbe mfupi wa maandishi nao haukujibiwa. Siku iliyofuata nilimuuliza mfanyakazi mwenzetu Bi Mariam Mkali, ambaye anaishi naye jirani katika nyumba za kampuni zilizoko Tabata Mawenzi, akaniambia ni kweli anaumwa lakini mara nyingi huwa hayupo nyumbani kwake.

Mapema wiki hii, Mpiga Picha wetu Mkuu, Yassin Kayombo akiwa chumba cha habari alisikika akisema Zahor ni mgonjwa na anaugulia kwa ndugu yake mmoja maeneo ya Chanika, hivyo tulimtaka afuatilie na kutujulisha mahali hapo ili tuweze kwenda kumjulia hali.

Ni juzi tu Kayombo alirudi na jibu na kutueleza mahali anapopatikana Zahor, lakini kabla ya kufanyika kwa taratibu za kwenda kumjulia hali, habari za simanzi ndizo zilizotufikia katika hali ya kustukiza na kutuacha na majonzi makubwa.

Zahor ambaye mpaka umauti unamkuta alikuwa ndiye Msanifu Mkuu wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo, binafsi nina historia ndefu naye, kwani tuliajiriwa wote katika Shirika la Magazeti ya Chama, tukiwa vijana wadogo baada ya kuhitimu elimu ya sekondari.

Wote tulianzia Dawati la Michezo lakini mwenzangu alikuwa mzuri zaidi katika uandishi wa habari za michezo, hivyo aliendelea kudumu katika dawati hilo, mimi nikihamishwa kwenda Dawati la Habari chini ya Mhariri mkongwe Joe Nakajumo.

Kutokana na uwezo wake, Zahor akiwa bado kijana mdogo mnamo Machi 14, 1997 aliaminiwa na Bodi ya Uhariri ya wakati huo, chini ya uongozi wa Kaimu Mhariri Mkuu Josiah Mufungo, kuwa Kaimu Mhariri wa Habari za Michezo  baada ya Godrey Lutego, kuacha kazi.

Miongoni mwa majukumu aliyopewa ni pamoja na kuwa kiongozi wa sehemu ya michezo na kwamba watendaji wote wa sehemu hiyo watawajibika kwake. Barua yake ya uteuzi ilimwelekeza pia atasimamia ukusanyaji wa habari, makala na picha zinazohusu michezo, burudani na sanaa na kuziwasilisha kwa Msanifu Mkuu kwa kuzingatia ‘dead line’ ya wakati huo.

Kimsingi msiba wa Zahor ambaye tulikuwa tukitaniana sana kutokana na ukweli kwamba ni miongoni mwa waandishi wa muda mrefu tuliosalia katika chumba cha habari cha Uhuru na Mzalendo, tulioajiriwa katika miaka 1990 tukiwa vijana wadogo.

Mara nyingi tulikuwa tukitaniana na kuitana majina tofauti tofauti kama vile Zungu, Baharia, Shemeji, vijana wa zamani, doctor na mengine mengi tu, ilihali tulikuwa ni watu tuliofahamiana sana na wenye kuheshimiana inapofika suala la kazi.

Tuliwahi kutaniana kwamba kwa kuwa tunafahamiana sana, basi siku mmoja wetu akiitwa mbele ya haki basi mwenzie amuandikie ‘orbituary’ yaani buriani kwa tafsiri ya haraka haraka na kweli baada ya kupata taarifa za kifo cha ‘Doctor’niliona pamoja na makujumu yangu mengi kwa sasa, lakini nawajibika kuandika hii buriani kumuenzi mwenzangu ambaye nimedumu naye ndani ya chumba cha habari cha Uhuru kwa takriban miaka 28 sasa.

Pamoja na kwamba Zahor hakuwahi kupata mafunzo ya muda mrefu ya tasnia ya uandishi wa habari, lakini uwezo wake wa uandishi ulijengeka siku hadi siku kutokana na mapenzi aliyokuwa nayo katika fani hiyo, pamoja na usaidizi mkubwa alioupata kutoka kwa Wahariri wakongwe kwenye chumba cha habari cha Uhuru kuanzia pale Pugu Road sasa Nyerere na baadaye Lumumba ambako ndiyo makao makuu ya Uhuru Publications Ltd hadi sasa.

Miongoni mwa Wahariri wakongwe ‘walimpika’ Zahor ‘Ramoza’ ni Marehemu Ahmed Shimye, Masoud Saanani, Lutego kwa upande wa habari za michezo na Nakajumo, Mwadini Hassan na Jacqueline Liana. Wengine ni Said Nguba na Mufungo ambao kwa nyakati tofauti waliongoza kampuni ya Uhuru Publications.

Kutokana na ‘kupikwa’ na Wahariri hao wachache niliowataja Zahor, alichipukia kuwa mwandishi mzuri si kwa habari za michezo, bali hata katika dawati la habari za kawaida na uandishi wa makala.

Ndani ya chumba cha habari waandishi wengi walipenda kumtania kwa kumwita ‘Doctor’ si kwa sababu alikuwa na ufahamu wowote kuhusiana na masuala ya tiba, bali kutokana na uwezo wake wa kumudu madawati yote kiutendaji. Ni miongoni mwa waandishi wa habari wachache wenye uwezo wa kutumika katika madawati yote pasipo kutiliwa shaka.

Binafsi nilipenda kumwita ‘kiraka’ kwani kila upungufu ulipojitokeza katika eneo fulani nilimuomba Zahor asaidie na kazi zilikwenda bila matatizo.

Mfano mzuri ni jinsi alivyoweza kumudu uandaaji wa matoleo maalumu ya shughuli za Chama, ikiwemo mikutano mikuu, kampeni na habari za bunge. Kutoka na uwezo  na uzoefu wake, Bodi ya Uhariri haikusita kumpa nafasi ya kuwa Msanifu Mkuu, ambaye kwa utaratibu wa uendeshaji wa vyombo vya habari hususan magazeti ndiye ‘chujio la mwisho’ kabla ya habari au makala kwenda kwa mchapishaji.

Daima tutamkumbuka Zahor kutokana na umakini na uwajibikaji wake anapokuwa kazini, kwani anapokaa katika dawati  alikuwa si mtu wa kuzurura au kuongea sana, bali alihakikisha anamaliza kazi yake kwa muda na anapohakikisha gazeti limetumwa kiwandani alikuwa akichukua magazeti na kuondoka.

Alipenda sana sanaa, michezo na burudani hususan muziki wa bendi na hasa nyimbo za zamani zilizoimbwa na kina Marijani Rajab, Mbaraka Mwinshehe na aliwahi kuwa Mshauri wa Bendi ya Sikinde wa masuala ya habari.

MHARIRI CHIFU JOE aeleza alivyomfahamu Zahor

Akiwa kwenye chumba cha habari jana Chief Joe alikuwa miongoni mwa waandishi waliopekea taarifa za kifo cha Zahor na alimwelezea kwamba marehemu Zahor ni Mwandishi wa habari aliyefunzwa na kulelewa na magazeti ya Uhuru na Mzalendo.

Tangu ujana wake hadi umauti ulipomfika jana alikuwa anayatumikia magazeti ya Uhuru na Mzalendo katika vitengo mbalimbali.

Zahor alikuwa na kipaji cha utunzi wa hadithi na ndicho kilichomfanya aungane na magazeti haya.

Alianza kutunga hadithi na kuzileta kuchapishwa katika gazeti la Mzalendo miaka ya 1980 mwishoni wakati huo akiwa mwanafunzi wa shule ya sekondari.

Miongoni mwa hadithi za kusisimua aliita ‘Uliyataka Mwenyewe’. Hadithi hii ilimwelezea kijana aliyemtaja kwa jina la Ramoza jinsi alivyokutana na msichana Anie. Ramoza ni kifupi cha majina yake ambayo ni Rashid Mohammed Zahor.

Hadithi hiyo ilitoka mfululizo katika gazeti la Mzalendo kila Jumapili kuanzia Mzalendo ya Jumapili Februari 7, mwaka 1993 na kumalizia katika Mzalendo ya Jumapili ya Februari 28.

Tangu nilipomfahamu wakati huo, Zahoro ambaye alikuwa ni kijana mtaratibu na mwenye kupenda kujifunza, alikuwa anakuja kwenye ofisi za magazeti barabara ya Pugu, sasa inaitwa Nyerere kuleta hadithi.

Kwa kuwa alikuwa ni mtunzi mzuri wa hadithi za kusisimua na tayari alikuwa ameyafahamu na kuyazoea mazingira ya utendaji kazi ndani ya chumba cha habari, uongozi wa Shirika uliamua kumuajiri. Katika ajira yake mpya alianzia kitengo cha habari za michezo.

Jane Mihanji amlilia Zahor

Zahor alikuwa akiniita dada siku zote, akinipa heshima ya jinsia yangu na ukaribu wetu katika utendaji kazi. Akiwa msanifu mkuu wa magazeti yetu, nilikuwa msaidizi wake. Pamoja na kwamba alikuwa bosi wangu, hakuwai kuleta dharau  kutokana na nafasi yake.

Alikuwa ni mtu mcheshi na mara zote akiniona baada ya salaamu lazima ilikuwa achomeke utani wa jambo fulani, tukikumbuka maisha ya zamani ya chumba cha habari na viongozi wetu ambao wengi wamestaafu.

Zahor alikuwa ni mchapakazi na aliipenda kazi yake. Hata nilipokuja kupanda cheo na kuwa Naibu Mhariri katika magazeti yetu, aliona tu kuwa ni sehemu wa mgawanyo wa majukumu. Aliendelea kunipa heshima kama dada yake na kiongozi wake. Nami pia wakati nikiwa na nafasi hiyo, sikuwa nimeacha kuhariri, kwa hiyo mara zote tulikuwa tukikutana kwenye kazi.

Ni mtu aliyekuwa akipenda kujifunza, kwani alianza katika uandishi wa hadithi, lakini kwa vile alikaa muda mwingi na waandishi wa habari, alijikuta akianza kuandika habari za michezo na baadaye ‘hard news’ hadi kuja kupewa majukumu makubwa ya usanifu.

Kwa mujibu wa familia ya marehemu Zahor anatarajiwa kuzikwa leo katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar er Salaam.

Ninachoweza kusema Zahor ameitendea haki fani ya uandishi wa habari, kwani ameshiriki kikamilifu katika kuboresha kazi za uandishi wa habari ndani ya chumba cha habari cha Uhuru, akiwa Mhariri wa Michezo, Mhariri wa Burudani na hatimaye Msanifu Mkuu wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo.

Mwenyezi Mungu awape wepesi ndugu na jamaa wa marehemu Zahor katika kipindi hiki kigumu wanachokipitia kutokana na kifo cha mpendwa wao.

Kwa kheri ‘Doctor’ mwendo umeumaliza kwa kishindo.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji’un

Na Ramadhani Mkoma

admin

admin

Stay Connected test

  • 139 Follower
  • 204k Subscriber
  • 23.9k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

August 7, 2023
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • Afya Makala
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Sports
  • Uncategorized

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In