Mhe. Katambi ameyasema hayo Februari 5, 2024 bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Segerea (CCM), Mhe.Bonnah Kamoli ambaye amehoji lini kanuni mpya za malipo ya pensheni kwa wastaafu ya kila mwezi ya kutoka asilimia 50 hadi 67 itaanza kutumika.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Katambi amesema kupitia gazeti la serikali namba 357 la Mei 20, 2022 ilitangaza kanuni hiyo iliboresha kiwango cha mafao ya pensheni ya kila mwezi kwa wastaafu.
Amesema kanuni hizo ziliandaliwa kwa kushirikisha wadau wote (Serikali, Wafanyakazi na Waajiri) kwa lengo la kufanya maboresho ya pensheni ili kuwianisha mafao ya wanachama na kuifanya mifuko kuwa endelevu.
