Wednesday, May 21, 2025
English English Kiswahili Kiswahili
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • English English
  • Kiswahili Kiswahili
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result
Mwanzo MICHEZO

PABLO APEWA MITIHANI MIWILI SIMBA

>> Chama asimamisha mkutano

admin by admin
November 22, 2021
in MICHEZO
0 0
0
PABLO APEWA MITIHANI MIWILI SIMBA

KOCHA wa Simba, Pablo Franco

0
SHARES
192
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

BAADA ya kuanza vyema katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Ruvu Shooting, kwa kuichapa mabao 3-1, Kocha wa Simba, Pablo Franco raia wa Hispania, amepewa mitihani miwili ndani ya klabu hiyo.

Uongozi wa Klabu ya Simba, umempa kocha huyo mtihani wa kwanza kuhakikisha anaifikisha timu katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika na mtihani wa pili ni kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara walioutwaa mara nne mfululizo.

Akizungumza Dar es Salaam, katika mkutano wa klabu hiyo uliofanyika ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Barbara Gonzalez, alisema kipaumbele cha kwanza ambacho wamempa Kocha Pablo ni kuhakikisha wanatinga nusu fainali ya Kombe la Shirikisho na kutetea taji la ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Barbara alisema licha ya kutolewa Ligi ya Mabingwa Afrika, ila bado wanahitaji kufanya vizuri katika michuano hiyo katika msimu huu.

“Malengo yetu msimu huu ilikuwa ni kutetea ubingwa, kufika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa lakini tumeteleza, hivyo Mwenyezi Mungu ametupa nafasi nyingine katika Kombe la Shirikisho, kocha tunaye na naamini tutafikia tunapopataka,” alisema Barbara.

Aidha, Barbara alimpongeza aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Mohammed Dewji ‘Mo’, kwa mafanikio waliyoyapata chini ya uongozi wake kwa kushinda mara nne mataji ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

MO APEWA URAS SIMBA

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ alimtangaza Mwekezaji wa klabu hiyo Mohamed Dewji ‘Mo’ kuwa rais wa heshima ndani ya Simba kutokana na mambo mazuri anayoendelea kuyafanya.

Try Again alisema Simba imempa heshima hiyo Mo kutokana na mchango wake mkubwa alioufanya na anaoendelea kuufanya ndani ya klabu ya Simba.

“Kwa kutambua mchango wake mkubwa na makubwa aliyotufanyia katika klabu hii, kwa mapenzi ya dhati, katika kikao cha bodi kilichokaa hivi karibuni, bodi imeamua kumpa urais wa heshima Mo,” alisema Try Again.

Hata hivyo, aliongeza mabadiliko yamekamilika na mwekezaji Mo ameshaweka sh. bilioni 20 na watapata sh. milioni 200 kila mwezi kwa ajili ya shughuli za klabu.

Wakati huo huo  aliyekuwa mchezaji wa Simba kwa sasa anakipigia Berkane ya Morocco, Clatous Chama alisimamisha kwa muda hotuba ya ‘Try Again’ katika mkutano mkuu wa klabu hiyo baada ya kutajwa jina lake.

Wanachama walilipuka kwa furaha wakati Try Again alipowaeleza kwamba wana uwezo wa kumsajili mchezaji yoyote wanayemtaka baada ya mwekezaji wa klabu hiyo, Mo kumhakikishia fedha zipo.

“Tutamleta yeyote katika usajili, sijui awe Chama au nani, kwani Mo ametuhakikishia kuwa hela ya kufanya usajili ipo yakutosha,” alisema Try Again Baada ya kauli hiyo, wajumbe waliohudhuria katika mkutano huo, walilipuka kwa shangwe wakiamini ni taarifa nzuri kwao.

Hali hiyo iliyosababisha Try Again kusimama kwa sekunde chache kusubiri wanachama wamalize kushangilia na baadaye aliendelea na hotuba yake.

KASSIM DEWJI AMRITH HANS POPPE

Mwenyekiti wa bodi Try Again alimtangaza Kassim Dewji kuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo.

Dewji anachukua nafasi ya Zacharia Hans Poppe aliyefariki Septemba mwaka huu na kuzikwa mkoani Iringa.

“Tunafahamu uwezo Dewji, hivyo bodi imemkabidhi jukumu la kuongoza kamati ya usajili ambayo ilikuwa chini ya Hans Poppe enzi za uhai wake,” alisema Try Again

ZUNGU AFUNGUKA

Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, alisema mpira una gharama na gharama za mpira sio uwekezaji wa pesa bali ni kupata machungu ya kufungwa.

“Tusitegemee kuwa timu yetu haitafungwa, kuna mambo mengi yanayofanya timu ifungwe, kuna mambo ya makusudi, uzembe lakini kuna kuzidiwa na muda mwingine wachezaji kuchoka kwa hiyo tushinde pamoja na tufungwe pamoja sio tukishinda uongozi mzuri na tukifungwa viongozi wabaya, tujue kuwa viongozi ndio wanatusaidia,” alisema.

Hata hivyo Zungu aliwataka viongozi kuhakikisha wanawaambia makocha wapya wanaokuja kuwa huku sio ulaya, hivyo wahakikishe wanawajenga wachezaji kisaikolojia ili timu ifanye vizuri.

Katika mkutano huo Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu ameweka wazi kuwa, klabu ina mpango wa kujenga ukumbi wa mikutano na ofisi katika jengo lao lililopo Mtaa wa Msimbazi.

“Awali jengo hilo ambalo ni moja ya vitega uchumi vya klabu, lilikuwa likiingiza sh. milioni 200 kwa mwaka, lakini kwa sasa linaingiza sh. milioni 500, tumezungumza mwekezaji ili klabu ijenge ofisi na ukumbi katika jengo hilo na mchakato wa ujenzi utaanza Januari mwakani,” alisema Mangungu.

Wanachama wa klabu ya Simba walitumia saa mbili katika mkutano mkuu ulioanza saa 4:02 asubuhi na kufikia tamati saa 6:00 mchana, wanachama wa klabu hiyo walijadili ajenda 10 kati ya 11 ambazo zilianishwa awali.

Ajenda ambayo haikujadiliwa ni ya kupokea na kujadili mapendekezo ya marekebisho ya kanuni za uchaguzi na katiba ya klabu.

Kati ya ajenda 10 zilizojadiliwa katika mkutano huo uliofunguliwa na Zungu aliyekuwa mgeni rasmi, ni hotuba ya mwenyekiti, kupokea na kujadili taarifa ya utendaji kutoka bodi ya wakurugenzi na kupokea taarifa ya fedha zilizokaguliwa za mwaka uliopita 2020.

TAARIFA YA FEDHA

Mkuu wa Fedha, Utawala na Utendaji wa Simba, Yusuph Nassor alisoma taarifa ya fedha na kusema mwaka jana klabu iliingiza sh. bilioni 12.1 na matumizi ilikuwa sh. bilioni 12.3.

“Mo alitoa sh.bilioni 5.2 ambayo inakaribia nusu ya bajeti ambayo ni nje ya sh. bilioni  20 za uwekezaji, mwaka huu wa fedha klabu itaingiza sh. bilioni 11.8,” alisema Yusuph bila kutaja matumizi ya mwaka huu wa fedha.

Alisema katika fedha hizo, Mo ataingiza sh. bilioni 5.1 na tayari ameshatoa sh. bilioni 1.5 na sh. bilioni 1.2 zilitumika katika usajili.

Hata hivyo aliongeza klabu hiyo kama inahitaji kupambana kimataifa inapaswa kuongeza bajeti yake kwani haiwezi kushindana na klabu zenye bajeti ya zaidi ya sh. bilioni 80.

Simba itaikaribisha Red Arrows ya Zambia katika mchezo wa kwanza wa mtoano wa Kombe la Shirikisho Afrika, utakaochezwa Novemba 28, mwaka huu katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kabla ya marudiano nchini Zambia Desemba 5, mwaka huu.

Na NASRA KITANA

admin

admin

Stay Connected test

  • 139 Follower
  • 204k Subscriber
  • 23.9k Follower
  • 99 Subscriber
  • Trending
  • Comments
  • Latest
MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

MADAKTARI WAELEZEA JINSI YA KUZUIA MIMBA ISIHARIBIKE

July 9, 2021
BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

BREAKING NEWS: RATIBA LIGI KUU NBC MSIMU WA 2023/2024 HII HAPA

August 7, 2023
TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

TABWA YAMSIFU SAMIA KUWAPA FURSA WANAWAKE

July 9, 2021
BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

BEI MPYA YA MBAAZI, KUNDE YAWAPANDISHA MZUKA WAKULIMA

August 9, 2021
NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

NDUGU MATATANI KUMSHAMBULIA, KUMJERUHI MWENZAO KISA NG’OMBE

0
WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMEKUA WAKIIKOSEA SERIKALI KWAKUTOA TAARIFA ZA UONGO

0

OFISA ELIMU, MHANDISI, MKUU WA SHULE WAKALIA ‘KUTI KAVU’

0
STENDI YA ZAMANI UBUNGO  KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

STENDI YA ZAMANI UBUNGO KUJENGWA DEPO MABASI MWENDOKASI

0
TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 11, 2024

November 11, 2024
YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 1, 2024

October 31, 2024
Instagram Youtube Twitter Facebook

We are a diverse team of experts, innovative thinkers, creative designers, writers, innovators, strategists, pyschologists, comunictaors and web developers. UMG is extremely passionate about growing clients’ businesses, helping them achieve their goals and making a difference by raising the creative and communications industry standards in Tanzania.

Follow Us

Browse by Category

  • Afya Makala
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • RIWAYA
  • SIASA
  • Sports
  • Uncategorized

Recent News

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

TALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 20, 2024

November 20, 2024

YALIYOJIRI KATIKA GAZETI LA UELEKEO LEO NOVEMBA 12, 2024

November 12, 2024

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In