Sunday, July 5, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

admin by admin
May 20, 2022
in Habari Kitaifa
0
MIPAKA YA TANZANIA IPO SHWARI

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Stergomena Tax.

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Stergomena Tax, amesema hali ya ulinzi na usalama katika mipaka ya Tanzania yenye urefu wa kilometa 5,461.20 na kuhusisha eneo la nchi kavu na majini, ipo shwari

Mipaka hiyo ni baina ya Tanzania na Msumbiji, Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa wizara hiyo katika mwaka wa Fedha 2022/2023, Waziri huyo amesema katika kipindi hicho hapakuwa na matukio ya uhasama yaliyoripotiwa baina Tanzania na nchi zinazopakana, licha ya kuwepo changamoto kadhaa.

MPAKA WA TANZANIA NA DRC

Stergomena alisema hali ya usalama wa mpaka huo ni shwari kwani hakuna tukio la kuhatarisha usalama kwa nchi.

Hata hivyo, alisema ndani ya DRC yameripotiwa matukio ya waasi kushambulia miji mbalimbali nchini humo.

“Wizara kupitia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) imeendelea kuwa macho na kujipanga wakati wote. Aidha, ushiriki wa Tanzania katika misheni ya Umoja wa Mataifa (UN) katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (United Nations Organisation Stabilization Mission in the Democratic Republic of the Congo – MONUSCO) unaisaidia nchi kujiimarisha kiulinzi ipasavyo,” alisisitiza.

MPAKA TANZANIA NA MALAWI

Stergomena alieleza kuwa hali ya usalama ya mpaka huo ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama lililoripotiwa.

Alisisitiza kuwa ushirikiano uliopo baina ya Jeshi la Tanzania na Jeshi la Malawi ni mzuri na inajidhihirisha kutokana na mahusiano mazuri yaliyopo ambayo yamesababisha kufanyika michezo ya kirafiki kati ya timu za majeshi ya nchi hizi mbili yaliyofanyika Brigedi ya Kusini, Julai mwaka jana.

“Changamoto ya mpaka katika Ziwa Nyasa inaendelea kufanyiwa kazi kupitia Tume Maalum ya Usuluhishi (High Level Mediation Team) iliyoundwa na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

“Serikali yetu kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inaendelea kutumia njia za kidiplomasia ili kulipatia ufumbuzi wa kudumu suala hilo,” alieleza.

Kuhusu hali ya mpaka wa Tanzania na Zambia, alisema hali ya usalama katika mpaka huo ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama wa nchi lililoripotiwa hadi sasa.

MPAKA TANZANIA NA BURUNDI

Akieleza hali ya usalama wa mpaka huo, alisema hali ni shwari kwani hakuna matukio yoyote yaliyoripotiwa kuhatarisha usalama baina ya nchi hizo, ingawa eneo hilo linakabiliwa na uwepo wa wahamiaji haramu, uvamizi wa wakulima na uingizaji wa mifugo kwa ajili ya kupata malisho ambapo JWTZ imeendelea kukabiliana na hali hiyo.

MPAKA TANZANIA NA RWANDA

Waziri huyo wa ulinzi alisema usalama wa mpaka huo ni shwari, ingawa yapo matukio machache ya kihalifu ya wahamiaji haramu na uingizaji wa mifugo kwa ajili ya malisho. Wizara kupitia JWTZ inaendelea kuchukua hatua za kudhibiti matukio hayo.

MPAKA TANZANIA NA UGANDA

Stergomena alibainisha kuwa hali ya usalama katika mpaka huo ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama wa nchi.

Hata hivyo, alieleza uwepo wa changamoto ya uingizaji haramu wa mifugo kwa ajili ya malisho.

Alisema juhudi za kuimarisha mpaka zinaendelea kwa kuongeza alama kati ya marundo ya mawe yaliyowekwa na mkoloni, na kujenga barabara ya usalama kwenye Mpaka

MPAKA TANZANIA NA KENYA

Alieleza kuwa hali ya usalama wa mpaka baina ya Tanzania na Kenya ni shwari na hakuna tukio la kuhatarisha usalama dhidi ya Tanzania lililoripotiwa.

Alibainisha kuwa ipo changamoto ya kuharibiwa kwa alama za mpaka na kazi ya kuimarisha mpaka huo inayotekelezwa na timu ya wataalam kutoka Tanzania na Kenya inaendelea vizuri, ambapo awamu ya kwanza imeanzia eneo la Serengeti hadi Ziwa Natron.

MPAKA WA TANZANIA BAHARI YA HINDI

Kuhusu mpaka wa Tanzania katika Bahari ya Hindi, alisema hali yake ni shwari.

Waziri huyo alieleza kuwa katika mpaka huo Tanzania imepakana na nchi za Comoro na Shelisheli.

“Hakuna tukio lililoripotiwa la kuhatarisha usalama dhidi ya Tanzania. Aidha, JWTZ imeendelea kufanya doria za mara kwa mara katika eneo la Bahari ya Hindi ili kubaini na kuzuia wahamiaji haramu, usafirishaji haramu wa binadamu, usafirishaji wa dawa za kulevya na matishio ya kigaidi,” alibainisha.

MPAKA WA TANZANIA NA MSUMBIJI

Kwa mujibu wa waziri huyo wa ulinzi, alisema hali ya usalama wa mpaka huo ni ya wastani kutokana na mashambulizi yanayofanywa na kundi la kigaidi la Ansar Al Sunna Wal Jamaah (AASWJ) maeneo ya Kaskazini mwa Msumbiji, katika Jimbo la Cabo Delgado linalopakana na Mkoa wa Mtwara.

Alisema kundi hilo limekuwa likiathiri usalama kwa kuharibu na kupora mali za wananchi.

“Katikakupambananachangamoto hii, JWTZ imeendelea kuimarisha ulinzi kwa kufanya operesheni za ndani ya nchi kukabiliana na kundi hilo. Aidha, JWTZ inashiriki operesheni chini ya Mwamvuli wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika nchini Msumbiji (SADC Mission in Mozambique – SAMIM) katika jitihada za kudhibiti ugaidi.

Aliongeza kuwa: “Operesheni hizi zimeendelea kuimarisha ulinzi katika eneo la Mpaka, kudumisha amani na utulivu.”

Stergomena alisema operesheni hizo zimesaidia kupunguza nguvu ya kundi hilo la kigaidi, hata hivyo, kundi hilo linatekeleza mashambulizi kwa kuhamahama na kubadili mbinu za kimapigano.

Licha ya hali hiyo, alisema Tanzania inaendelea kupambana kuhakikisha kundi hilo halileti madhara zaidi.

“Wizara inaishukuru Serikali hususani, Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa kipaumbele katika kupambana na suala hili, kutoa fedha kwa ajili ya mahitaji mbalimbali yanayosaidia vikundi vya ulinzi kupambana dhidi ya kundi hilo,” alieleza.

Stergomena alisema katika mwaka wa fedha 2022/2023, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, imelenga kutekeleza mpango na bajeti kwa kuzingatia mambo Dira na Dhima ya Wizara, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22 – 2025/26).

Aliyataja mambo mengine yatakayozingatiwa katika bejeti hiyo ni Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030 (SDGs), Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020 na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.

Alibainisha kuwa katika mwaka huo wa fedha, serikali inatarajia kutenga fedha kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo, jumla ya sh. trilioni 2.7 ambapo kati ya fedha hizo, sh. trilioni 2.4 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. bilioni 230.3 kwa ajili ya kugharamia shughuli za maendeleo.

Na MUSSA YUSUPH, DODOMA

Previous Post

SERIKALI YATOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU

Next Post

MAHAKAMA KUU YAAMURU MKURUGENZI KULIPA BIL. 145/-

admin

admin

Next Post
KITUO MAALUMU CHAANZISHWA KUSHUGHULIKIA KESI ZA MIRATHI, NDOA, FAMILIA DAR

MAHAKAMA KUU YAAMURU MKURUGENZI KULIPA BIL. 145/-

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved