Saturday, July 4, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

MOTO MADINI UKO PALEPALE

Maagizo>>> Shughuli za uchimbaji, uchenjuaji na uchakataji madini zisimamiwe vizuri

admin by admin
December 14, 2021
in Habari Kitaifa
0
MOTO MADINI UKO PALEPALE

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akishuhudia tukio la Utiaji Saini makubaliano kati ya Serikali na Kampuni za Uchimbaji Madini za Black Rock Mining Limited, Strandline Resources Limited

RAIS Samia Suluhu Hassan, amewahakikishia Watanzania kuwa, moto katika kulinda madini hautazimika na kwamba serikali yake ipo macho kwa kila hatua itakayofanikisha nchi kunufaika zaidi na rasilimali hiyo.

Amesema hawezi kuruhusu uhujumu, wizi na utoroshaji wa madini, hivyo ameiagiza Wizara ya Madini kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, kuhakikisha hatua zinachukuliwa ikiwemo kufanya doria za mara kwa mara ili kuimarisha ulinzi.

Aidha, ameeleza kuwa, pamoja na kuimarika kwa udhibiti wa utoroshaji wa madini katika viwanja vya ndege, bandari na maeneo ya mipakani, anazo taarifa bado kuna utoroshaji wa madini katika baadhi ya maeneo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, katika utiaji saini makubaliano kati ya serikali na kampuni nne za uchimbaji madini, Rais Samia alisema mafanikio hayo ni safari ambayo hakuianza yeye, bali ilianzwa na mtangulizi wake, Hayati Rais Dk. John Magufuli na kusisitiza kwamba moto wa kulinda madini hautazimika kwa kuwa serikali yake ipo macho katika kila hatua itakayofanikisha nchi kunufaika na rasilimali hiyo.

“Serikali iliamua kufanya mabadiliko makubwa ya sheria zinazosimamia madini, ili kusaidia kumiliki rasilimali hizo kwa niaba ya wananchi na maslahi ya taifa,” alisema.

Rais Samia alisisitiza makubaliano yaliyofikiwa kati ya serikali na kampuni za uchimbaji wa madini, ni matokeo ya jitihada hizo kwa kuwezesha kuwa na ubia baina ya mwekezaji na serikali.

Aliongeza kuwa, miradi hiyo itaiwezesha serikali kupata tozo, ajira, gawio na ukuzaji wa huduma kwa kampuni na kurudisha hisani kwa wananchi.

“Ni wajibu wetu kuhakikisha shughuli za uchimbaji, uchenjuaji na uchakataji wa madini, zinasimamiwa vizuri. Hivyo wizara isimamie kikamilifu uongezaji wa thamani kwa kuwa haliepukiki. Leo kuna kampuni ilikuwa isaini hapa wakakataa kipengele cha uongezaji thamani, ninawapa wizara uwezo wa kusaini nao, lakini nisisitize tutachimba kuchenjua na kuongeza thamani hapa nchini,” alisema.

Rais Samia alisema hatua hiyo itasaidia fedha nyingi kubaki nchini na kwenda na mnyororo wa thamani.

Rais Samia alisisitiza sekta ya madini imeendelea kukua na kuongeza mchango wake katika pato la taifa, lengo ni kufikia mwaka 2025 sekta hiyo ichangia asilimia 10.

Alisema kutokana na hali iliyopo ambapo kwa sasa imefikia asilimia 6.7, ni wazi malengo hayo yatafikiwa.

Hata hivyo, Rais Samia alisisitiza kuwa na madini pekee si utajiri bali kuchimba, kuongeza thamani na kuchenjua, hivyo alifurahi kusikia wawekezaji walioingia mkataba wamekubali kupewa leseni na kuridhia kuhusu kuongeza thamani nchini.

Alisema ili kuhakikisha nchi inanufaika na rasilimali hiyo, ni vyema usimamizi na udhibiti wa madini katika viwanja vya ndege, bandarini na mipakani uimarishwe.

Rais Samia aliwataka waliopewa dhima ya kuzuia utoroshaji wa madini, kuwa wazalendo na kutokuwa chanzo cha utoroshaji.

“Nipongeze timu za majadiliano, haikuwa kazi rahisi, hata kuwa hapa si haba, mlikwenda mlishindwa mkarudi hadi kufikia leo, bado kuna mambo madogo madogo lakini kila yatakavyojitokeza mjitahidi kurudisha kwenye mstari,” alisema.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akishuhudia makabidhiano ya Hati baada ya tukio la kusaini makubaliano kati ya Serikali na Kampuni za uchimbaji Madini za Black Rock Mining Limited, Strandline Resources Limited na Nyanzaga katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Convention Centre Jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU

UTOROSHAJI MADINI

Alisema pamoja jitihada hizo, zipo taarifa katika baadhi ya maeneo wahujumu kwa kushirikiana na watendaji wasiokuwa waaminifu, kunafanyika wizi hivyo aliwataka wanaosimamia wahakikishe hakuna madini yanayotoroshwa.

Rais Samia alisema kazi hiyo haiwezi kufanikiwa kwa kuachia vyombo vya dola pekee, bali wananchi watoe taarifa wanaposhuhudia mienendo isiyofaa.

“Vyombo vya ulinzi na usalama pia tulinde kila kona ili kuimarisha uchumi wetu, hali hii haikubaliki. Naigiza wizara  kuongeza nguvu katika wizi na utoroshaji wa madini kwa kufanyika doria za mara kwa mara ili kujua wahusika na hatua zinaozchukuliwa,” alisema.

Alisema matarajio yake ni kuona makubaliano yaliyofikiwa utekelezaji wake unafanyika kwa haraka na kuleta manufaa kwa wananchi.

Alisisitiza kuwa kampuni hizo zitafanya uwekezaji wa zaidi ya sh. Trilioni 1.7 na kuongeza mapato jambo alilosema litatoa fursa za ajira, gawio na kuimarisha uchumi.

Rais Samia alieleza kuwa, miradi hiyo ikishirikisha wananchi ipasavyo wakati wa kupanga na kugusu maslahi yao itaondoa migogoro.

“Wasipokuwa na uelewa ndio matatizo yanaanza, nina taarifa kuwa mradi wa kuchimba mchanga Kigamboni una shida na wananchi wa Kigamboni hawapo hapa na walishaanza vurugu kupitia kwa diwani wao,” alisema.

Aliongeza kuwa ”Diwani huyo inamfanya kuwa na alama ya kuuliza kwa kuwa hata wakati wa operesheni ya Machinga ndio diwani pekee aliyehamasisha vurugu ili wasiondoke na sasa ameongoza tena wananchi kufanya vurugu kwa sababu hawajaelewa wakielimishwa wataulinda kwa kuwa mapato yatokanayo ndio watafaidika,”alisema.

AWAKUMBUSHA WAWEKEZAJI

Aidha, aliwakumbusha wawekezaji kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na utunzaji wa mazingira hususan katika uchimbaji wa mchanga baharini.

Rais Samia alisema ni muhimu wasimamizi wa mazingira wakiwemo NEMC, wakaguzi wa uchimbaji na wawekezaji kuwa makini kwa kuwa, kusubiri madhara yatokee ili watoze faini na kukusanya fedha si malengo.

Alisema urudishaji wa fadhila kwa wananchi sio hiyari kwani ni haki yao, hivyo wahakikishe wanafikiwa ipasavyo.

“Wakuu wa wilaya, serikali za mitaa na wasimamizi acheni ubabe migodini sio mnaenda kuchukua fedha za fadhila kwa wananchi na kutumia kwa mambo mengine, lakini wabunge miradi hii ikawasaidie kujenga maendeleo ya nchi sio iwajenge nyie binafsi. Mambo ya kwenda kutisha kama si mimi msingepata kwa hiyo mimi nina ngapi hapana,” alisema.

Alisisitiza kuwa sera na sheria zimefanyiwa marekebisho kwa mtazamo wa kuvutia wawekezaji, hivyo anataka kuona wawekezaji wakubwa ambao watapandisha hadhi ya nchi wanafunguliwa milango.

Na MARIAM MZIWANDA

Previous Post

WAKAZI 3900 WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI

Next Post

DK. MWINYI ASHUSHA MAAGIZO TUME YA MAADILI YA VIONGOZI

admin

admin

Next Post
DK. MWINYI ASHUSHA MAAGIZO TUME YA MAADILI YA VIONGOZI

DK. MWINYI ASHUSHA MAAGIZO TUME YA MAADILI YA VIONGOZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved