Saturday, July 4, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

YANGA NI KICHEKO TU LEO

MASTAA wapya, Koffi Olomide kuwasha moto

admin by admin
October 26, 2021
in MICHEZO
0
YANGA NI KICHEKO TU LEO

Feisal Salum

KAMA kuna watu ambao watakuwa na kicheko basi ni mashabiki, wapenzi na wanachama wa klabu ya Yanga ya Jijini Dar es Salaam.

Pia, kama kuna watu ambao wanatembea kwa kuringa na kujisikia kutabasamu muda wote, ni hao hao mashabiki wa Yanga au ukipenda unaweza kuwaita Wananchi.

Hii inatokana na usajili mkubwa walioufanya kwa kujiandaa na msimu mpya wa mashindano ya 2021/2022 ambayo yanatarajia kuanza kutimua vumbi mwezi ujao.

Yanga imetuliza akili, imeumiza kichwa kwa kufanya usajili wa kutisha ili kuhakikisha inafanya vizuri uwanjani haswa wakiwa na lengo la kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara ambao wameukosa kwa miaka kadhaa mfululizo.

Leo litafanyika tamasha kubwa linalojulikana kwa jina la ‘Siku ya Mwananchi’, kuanzia saa 3:00 asubuhi, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kwa kuanza na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.

Baadae utapigwa mchezo kati ya Yanga na timu ya Zanaco  kutoka nchini Zambia.

WIKI ILIPOANZA

Ikumbukwe kuwa klabu ya Yanga ilianzishwa mwaka 1935, hii inakuwa mara ya pili kufanya tamasha kubwa kama hilo baada ya Agosti 30 mwaka jana kufanyika kwa mara ya kwanza na kufanya vizuri.

Tangu Jumatatu ya wiki hii, Yanga walikuwa na shughuli mbalimbali zinazoihusu klabu hiyo, ikiwemo kutambulisha jezi mpya, kutambulisha wasanii ambao watatumbuiza siku ya leo na leo ndio tamati ya yote waliyoyafanya kwa wiki nzima.

Yanga wakiwa katika maandalizi ya siku ya leo, huku wanachama, mashabiki wa timu hiyo wakitoa misaada mbalimbali nchi nzima  na kusafisha Hospitali, makaburi  nakufanya  kazi mbalimbali katika maeneo yao wanayoishi.

Sambamba na hilo, wapenzi na wanachama wa Kanda ya Temeke Mkoani Dar es Salaam walikwenda Hospitali ya Temeke na kutoa misaada na kufanya usafi.

Huku tawi la Yanga Temeke Mikoroshini likifanya usafi katika Makaburi ya Nurul Imani Kata ya Sandali wakiwa na Diwani wa CCM,Christopher Kabalika.

WASANII KIBAO AKIWEMO KOFFI OLOMIDE

Katika tamasha la leo, uongozi wa Yanga umeeleza kuwa  mwanamuziki mkongwe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DR), Koffi Olomide ‘Mopao’, atakuwa mmoja wa wasanii ambao watatumbuiza.

Mopao ambaye ametua nchini jana mchana, anasema amekuja Dar es Salaam kusimamisha nchi, atafanya tamasha bora zaidi kwa kuwa hata yeye ni mpenzi wa timu hiyo ambayo ni mabingwa wa Ligi Kuu Bara mara 27.

Wasanii wengine kadhaa ambao wameonesha utayari wa kujitokeza kwa wingi kusherehekea kwa pamoja na mashabiki wao ni Faustina Mfinanga ‘Nandy’ au ‘African Princess’, ametunga wimbo unaojulikana kwa jina la ‘Yanga’, ambao anatarajia kuutambulisha leo.

Wengine ambao watapamba tamasha hilo ni Billnas, Chege Chunga, Mheshimiwa Temba, Shishi Baby, Mzee wa Bwax, Juma Nature, Baba Levo, G Nako na wengine wataendelea kutambulishwa.

MECHI YA KIRAFIKI

Pia waliitangaza timu ya Zanaco kutoka Zambia, ndio watacheza nayo baada ya burudani kuisha na kuangalia soka kabambe kutoka kwa mastaa mbalimbali waliosajiliwa.

Jumatano iliyopita, pia walizindua jezi mpya kwa ajili ya msimu ujao ambazo mashabiki wamehimizwa kununua kwa wingi ili kuichangia timu yao.

Tukio lingine ambalo Yanga wamelifanya kwa wiki hii ni kumtambulisha, aliyekuwa Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, kuhamia katika klabu hiyo kama msemaji pia hivyoakiwa kitengo kimoja na Hassan Bumbuli ambaye walikuwa wakitupiana maneno kipindi cha nyuma.

WATAMKUBALI MANARA?

Kutokana na uwezo wa kuongea na mashabiki aliokuwa nao Manara akiwa Simba, wanachama na mashabiki wa Yanga walimchukia lakini leo kahamia katika klabu yao, na utambulisho wake utafanyika pia leo katika tamasha hilo.

Haji Manara

Kila mmoja leo ataondoka na jibu baada ya kutambulishwa Yanga, je mashabiki wamempokea Manara kuwa naye au wanamuona ni mpinzani wao kama ilivyokuwa awali, kwa kuwa aliwahi kusema hata wampe hela zote zilizopo benki kuu ya Tanzania, hawezi kuhamia Yanga.

Lakini sasa hivi amegeuka na kusema maneno yake sio msaafu wala biblia, yanaweza kubadilika muda wowote na wakati mwingine alikuwa anaongea vitu ambavyo hata yeye anaona haiwezekani kutokea.

MASTAA WATAKAVYO WASHA MOTO

Kuelekea tamasha hili, litakuwa maalum kwa kuwatambulisha mastaa wote wa Yanga ambao watacheza msimu wa 2021/2022.

Yannick Bangala

Kabla ya kuanza kwa mchezo dhidi ya Zanaco FC, kutakuwa na utambulisho wa wachezaji wapya na wale wa zamani akiwemo Mghana Godfrey Nyalko, ambaye atatmbulishwa kwa mara ya kwanza.

Utambulisho huo utawakosa nyota wapya, mlinda mlango raia wa Mali, djigui Diarra na Mganda Khalid Aucho ambao wameitwa timu zao za taifa.

Wachezaji ambao watatambulishwa ni makipa; Ramadhan Kabwili na Erick Johara.

Walinzi ni Djuma Shaaban, Kibwana Shomari, David Bryson, Adeyum Saleh, Yassin Mustapha, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, Dickson Job, Bakari Mwamnyeto na Yanick Bangala.

Viungo ni Mukoko Tumombe, Deus Kaseke, Feisal Salum ‘Feitoto’, Zawadi Mauya, Saido Ntibanzokinza, Farid Musa, Balama Mapinduzi, Jesus Moloko, Ditram Nchimbi na Dickson Ambundo.

Washambuliaji ni Fiston Mayele, Heritier Makambo, Yacouba Sogne na Yusuph Athumani.

Na ELIZABETH JOHN

Previous Post

IGP SIRRO AWASHUKIA VIKALI WANAOCHEZEA AMANI MITANDAONI

Next Post

SERIKALI YAANIKA MAFANIKIO, IDADI WALIOCHANJWA  KUJIKINGA CORONA YAONGEZEKA, MAPATO YAPAA

admin

admin

Next Post
SERIKALI YAANIKA MAFANIKIO, IDADI WALIOCHANJWA  KUJIKINGA CORONA YAONGEZEKA, MAPATO YAPAA

SERIKALI YAANIKA MAFANIKIO, IDADI WALIOCHANJWA  KUJIKINGA CORONA YAONGEZEKA, MAPATO YAPAA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved