Sunday, July 5, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

CCM YAPONGEZA MAONO YA SAMIA

admin by admin
September 2, 2021
in Habari Kitaifa
0
CCM YAPONGEZA MAONO YA SAMIA

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesifu hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan, kujali na kuwasilikiza wananchi kwa kushughulikia malalamiko yaliyotokana na tozo za miamala ya simu, kikimtaja kuwa na msimamo imara na thabiti.

Kimesema punguzo la tozo hizo ni unafuu kwa wananchi, ambao idadi kubwa wamekuwa wakitumia miamala ya simu kuendesha shughuli za kiuchumi na kusaidia wahitaji.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, wakati akizungumza na vijana wa taasisi ya mama yangu, nchi yangu inayoshughulika na uhamasishaji vijana.

Shaka alisema uamuzi huo umetolewa wakati mwafaka na kusisitiza kuwa pamoja na punguzo hilo, wananchi wanapaswa kufahamu wana wajibu wa moja kwa moja kuchangia maendeleo ya ujenzi wa taifa. Shaka alisema kitendo kilichofanywa na serikali chini ya Rais Samia, kimeonyesha uzalendo na uungwana kwa kuwajali na kuwasikiliza wananchi wake.

“CCM inampongeza Rais Samia kuwasikiliza wananchi kuhusu sakata la tozo za miamala ya simu, ambapo alitoa maelekezo ya viwango hivyo kutazamwa upya na sasa imepunguzwa kwa asilimia 30 huku kampuni zikipunguza kwa asilimia 10.

“Kazi ya kujenga nchi ni wajibu wa Watanzania wote bila kujali itikadi za kisiasa. Uamuzi huu ni upendo mkubwa alionao kwa wananchi anaowaongoza ili washiriki kuchangia maendeleo ya nchi yao kwa furaha,” alisema Shaka.

Hata hivyo, alibainisha wananchi wanapaswa kuelewa ni jukumu la kila mmoja kushiriki kazi ya ujenzi wa nchi na kuweka msukumo wa maendeleo na kupeleka huduma za jamii katika maeneo yote.

Aliwataka watendaji wa serikali kutambua kuwa kazi ya kumsadia Rais Samia katika kila eneo ni wajibu usiohitaji kuelelezwa wala kusukumwa, badala yake wautimize ipasavyo wakiweka mbele maslahi ya umma.

Shaka aliwataka Watanzania kupuuza uvumi unaoenezwa mitaani kuwa serikali ina mpango wa kusitisha elimu bila ada.

“Serikali ya Rais Samia itaendelea kugharamia elimu bila ada kwani unawagusa na kuwanufaisha wananchi walio wengi.

Zaidi itaendelea kutatua changamoto zilizokuwa zikikabili mpango huu ili wanafunzi wa Tanzania wapate elimu katika mazingira mazuri zaidi. Hivyo niwaombe wananchi wapuuze taarifa zinazodai serikali itausitisha,” alisema.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kundi hilo, Agness Maganga, alieleza kuwa wanamuunga mkono Rais Samia kwa kuwa serikali anayoiongoza imefanya mambo makubwa yakiwemo kupandisha madaraja watumishi wa umma 92000.

Pia kuondoa tozo ya asilimia sita ya kulinda thamani ya mkopo kwa wanufaika wa mkopo elimu ya juu, kuongeza bajeti ya mikopo elimu ya juu na kuendelea kutoa fedha kukamilisha na kuendeleza miradi mikubwa ya kimkakati nchini.

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, akizungumza na vijana wa taasisi inayoshughulika na uhamasishaji vijana ya Mama Yangu, Nchi Yangu, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam.

KAULI ZA WATOA HUDUMA ZA SIMU

Akizungumza na UHURU, Mwenyekiti wa Chama cha Watoa Huduma za Mitandao ya Simu Tanzania (TAMNOA), Hisham Hendi, alipongeza hatua ya serikali kufanya mazungumzo nao kujadili mbinu za haraka na muda mrefu katika ufanikishwaji wa azma ya serikali ya kuanzisha tozo ya mshikamano.

“Tunaipongeza serikali kupitia Wizara ya Fedha na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kufanya mazungumzo kadhaa na tasnia hii kujadili mbinu za haraka na za muda mrefu ili kufanikisha azma ya serikali kuanzisha tozo ya mshikamano na kujadili kwa upana ustawi wa sekta hii,” alisema.

Pia aliipongeza serikali kupunguza asilimia 30 ya tozo hiyo, huku wao wakiwa wamepunguza asilimia 10 na kuongeza kuwa, ni imani yao kuwa hatua hiyo zitarudisha wateja walioacha kutumia huduma hiyo au kufanya biashara.

Hendi ambaye pia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Vodacom, alibainisha kuwa katika katika enzi ya 4IR, sekta ya mawasiliano ina jukumu la kuziwezesha nyingine, zikiwemo ‘agritech’, ‘telemedicine’, malipo ya serikali na huduma katika kuendelea kuchangia ukuaji wa Taifa.

“Wanachama wa TAMNOA wamejitolea kuendelea kuwekeza katika ubunifu na uvumbuzi mpya lakini ili kufikia huko ni muhimu tuendelee kupata faida,” alisema.

Alisisitiza kuwa, ni muhimu kwa wadau wa sekta hiyo kufanya kazi kwa karibu na serikali, ili kujengeana maarifa juu ya ukusanyaji ushuru kupitia majukwaa ya kidigitali yanayofanya kazi kwa karibu na wadhibiti na wadau wengine kuhakikisha kufikiwa kwa malengo kwa usawa kati ya sekta binafsi na umma.

Na JUMA ISSIHAKA

 

Previous Post

WALIOSABABISHA MADHARA YA CHANJO KWA MIFUGO WASAKWA

Next Post

MBOWE AGONGA MWAMBA, AWASILISHA PINGAMIZI LINGINE

admin

admin

Next Post
MBOWE AGONGA MWAMBA, AWASILISHA PINGAMIZI LINGINE

MBOWE AGONGA MWAMBA, AWASILISHA PINGAMIZI LINGINE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved