Saturday, July 4, 2026
[gtranslate]
UMG
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
  • MAGAZETI
    • UELEKEO
  • UMG DIGITAL
  • UELEKEO DIGITAL
    • Instagram
    • Facebook
    • Twitter
    • Youtube
  • Mwanzo
  • UMG
  • Siasa
    • All
    • Business
    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    SHIRIKA LA OMUKA HUB NA NDI WAANDAA MAJADILIANO YA JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA SIASA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    WAZIRI JAFO ATETA NA WAKUU WA MIKOA

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU MWENYEKITI UVCCM AWAJIA JUU WANAOWACHAFUA VIONGOZI

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    MAKAMU WA RAIS DK. PHILIP MPANGO AKIONDOKA NCHINI ANGOLA

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    FORBES YAMTAJA TENA RAIS SAMIA.. “NI MIONGONI MWA WANAWAKE 100 WENYE UWEZO MKUBWA DUNIANI”

    Trending Tags

    • Trump Inauguration
    • United Stated
    • White House
    • Market Stories
    • Election Results
  • Biashara
    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    WAJASIRIAMALI WASHAURIWA KUTHIBITISHA UBORA WA BIDHAA NJOMBE

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML

    Trending Tags

    • Nintendo Switch
    • CES 2017
    • Playstation 4 Pro
    • Mark Zuckerberg
  • Burudani
    • All
    • Sports
    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    YANGA YAMNYATIA ABIALA KUTOKA CONGO DR

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

    SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0

  • Michezo
    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    SERIKALI YAAHIDI KUWAPELEKA MASHABIKI WA YANGA AFRIKA KUSINI

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    YANGA SC YAACHANA NA MOLOKO

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TETESI ZA SOKA BARANI ULAYA

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    TFF YAUFUNGIA UWANJA WA UHURU

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    BENCHIKHA; MCHEZO WA KESHO UTACHORA RAMANI KUELEKEA LIGI YA MABINGWA AFRIKA DHIDI YA WYDAD CASABLANCA

    Trending Tags

    • MotoGP 2017
    • eSports
    • Fashion Week
No Result
View All Result
UMG
No Result
View All Result

ZIARA YA RAIS SAMIA UFARANSA: WASOMI WAANIKA MAFANIKIO LUKUKI

>>KAMPUNI 60 za Ufaransa kuwekeza nchini, ulinzi bahari kuu kuimarishwa

admin by admin
February 16, 2022
in Habari Kitaifa
0
ZIARA YA RAIS SAMIA UFARANSA: WASOMI WAANIKA MAFANIKIO LUKUKI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza na kuagana na mwenyeji wake Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, katika Ikulu ya Elysée, Paris nchini Ufaransa.

SIKU moja baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kukamilisha ziara yake nchini Ufaransa, wataalamu mbalimbali wa masuala ya uchumi wa bahari, wanasiasa na balozi, wameonyesha matarajio makubwa ya mafanikio yatakayopatikana kutokana na ziara hiyo.

Miongoni mwa faida zilizotajwa kutokana na ziara hiyo ya Rais iliyomwezesha pia kuhutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Rasilimali Bahari Duniani ‘One Ocean Summit’ nchini humo, ni pamoja na kufungua fursa za uwekezaji.

Akizungumza na UHURU kwa njia ya simu, Balozi  wa Tanzania nchini Ufaransa,  Samwel Shelukindo, alisema ziara ya Rais Samia nchini humo ambayo imetokana na mwaliko wa Rais wa Ufaransa,  Emmanuel Macron, imekuwa na tija kwa diplomasia ya nchi hizo katika uchumi na uwekezaji.

Alisema kutokana na ziara hiyo, kampuni 60 kutoka nchini Ufaransa zimeitikia wito na zipo tayari kwa ajili ya uwekezaji Tanzania.

“Imekuwa ziara nzuri kuanzia mapokezi na mafanikio yaliyofikiwa, Ufaransa inaongoza kwa kuleta watalii wengi nchini Tanzania na  inaenda kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya uwekezaji,” alisema.

Balozi Shelukindo aliongeza kuwa, katika ziara hiyo, wakuu hao wa nchi mbili hizo, kwa pamoja walikubaliana mambo makubwa kadhaa, ikiwa ni pamoja na utayari wa Ufaransa kuisaidia Tanzania kupambana na uhalifu katika bahari kuu ili kuimarisha uchumi wa buluu.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Biashara wa Ufaransa, Frank Reicster, kabla ya kushuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika sekta mbalimbali kati ya Tanzania na Ufaransa katika mji wa Brest nchini Ufaransa, Februari 11, 2022.

Aidha, alieleza kuwa uchumi wa buluu ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania, hivyo Rais Macron amemuahidi Rais Samia kuwa nchi yake itafanya uwekezaji mkubwa katia sekta hiyo, ikiwemo kulinda uhalifu unaoweza kufanyika katika bahari kuu.

Alisema kati ya mikataba iliyotiwa saini kwa nchi hizo mbili ni pamoja na makubaliano kati ya Benki ya Kilimo Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa.

“Mkataba huo ni wa zaidi ya Euro milioni 80, ambapo utasaidia sekta ya kilimo, huku  mkataba wa ukarabati wa mindombinu na uwanja wa ndege wa terminal II, ikiwa ni muhimu ili kuimarisha sekta ya uchumi nchini,” alisema.

Alieleza kuwa, baada ya ziara hiyo, Watanzania watarajie wawekezaji wengi kutoka Ufaransa kuanzia Mei, mwaka huu.

Balozi Shelukindo alisisitiza kuwa, mikataba hiyo itaanza utekelezaji wake hivi karibuni baada tu ya kutiwa saini,  kwa kuwa ilishafanyiwa tathimini.

WATAALAMU UCHUMI BAHARI

Kwa upande wa wataalamu mbalimbali wa uchumi kupitia rasilimali za bahari, walisema ziara hiyo na ushiriki wa Tanzania katika mkutano wa ‘One Ocean Summit’ walisema utaongeza ushirikiano na mataifa mengine katika kulinda rasilimali bahari na kufanyika tathimini ya uwezo wa kitaifa kukabiliana na changamoto za uchafuzi, hivyo kuundwa mkakati ya kukabiliana nazo.

Akizungumza na UHURU, Februari 15, 2022, mtaalamu wa sayansi ya mazingira, Profesa William Mwegoha, alisema sera ya mazingira nchini inatambua umuhimu wa kushirikiana na mataifa mengine katika masuala ya mazingira.

Alieleza kuwa uchafuzi wa mazingira, hususan bahari, hauna mipaka, huvuka kutoka nchi moja kwenda nyingine, ndiyo maana kunafanyika mijadala mbalimbali ili kutatua changamoto hizo kuanzia ngazi za kidunia.

“Nchi siyo kisiwa, bali ipo kwenye mfumo wa kidunia, kwa hiyo majadiliano mengi lazima yataanza katika hatua za kidunia ili kujenga ushirikiano katika mapambano na changamoto za mazingira,” alisema.

Alifafanua kuwa ni muhimu kwa nchi kushiriki, kwa kuwa athari zinazotokana na shughuli za binadamu, huenda zikaanzia nchi yoyote na kusambaa hadi katika taifa lingine.

“Kwa hiyo ile mikakati inayowekwa kwa ajili ya kukabiliana na masuala hayo lazima na sisi (Tanzania) tuwe tunashiriki kujenga au kulinda maslahi yetu,” alisema.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akishuhudia Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, akiweka saini moja ya mikataba ya ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali kati ya Tanzania na Ufaransa iliyowakilishwa na Waziri wake wa Biashara, Frank Reicster, katika mji wa Brest nchini Ufaransa, Februari 11, 2022.

Alisema maana ya Tanzania kushiriki mkutano huo ni kwamba inafanyika tathimini ya uwezo wa kila nchi kukabiliana na changamoto hizo, katika upande wa rasilimali na utaalamu.

Alibainisha katika mkutano huo, hufanyika majadiliano ya kukubalina namna ya kufanya na nchi gani inahitaji msaada upi kukabili changamoto ipi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kigoda cha Utafiti katika Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Amos Majule, alisema ushiriki wa Tanzania katika mkutano huo ni muhimu kutokana na uwepo wa mikataba ya kimataifa kuhusu bahari ambayo nchi imetia saini.

“Bahari inaunganisha nchi mbalimbali duniani na kuna mambo mengi yanafanyika katika bahari, kwa mfano uvuvi na tunajua kwamba shughuli nyingi zinazofanyika humo zinaleta athari katika mazingira,” alisema.

Alieleza mikutano ya namna hiyo huwa na mikataba ya makubaliano kwa kila nchi inayoshiriki katika utunzaji na uendelezaji wa bahari.

Alibainisha kwamba Tanzania kwa sehemu kubwa ipo karibu na Bahari ya Hindi, hivyo ni muhimu kushiriki mikutano hiyo.

“Kumekuwa na mmomonyoko wa bahari duniani, kwa hiyo dunia kwa ujumla kupitia vikao hivyo inazungumza na kupanga mikakati ya kupunguza au kuzuia changamoto zinazoikumba bahari,” alisema.

Aliongeza kwamba kilichozungumzwa na Rais Samia katika mkutano huo kuhusu kuzitaka nchi zilizoendelea kutoa ushirikiano katika kutatua changamoto za uchafuzi wa bahari ni jambo la msingi.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Dk. Tumaini Gurumo, alipongeza hatua ya Rais Samia kushiriki mkutano wa bahari nchini Ufaransa, akisema utafungua mambo mengi kwa taifa.

“Bahari ina mambo mengi ambayo yote ni maendeleo kuanzia uvuvi, utengenezaji meli, usafirishaji na hata uwepo wa madini ambapo nchi zilizoendelea zinachimba madini baharini,” alisema.

Dk. Tumaini ambaye ni mtaalamu wa sheria za bahari, alisema hii ni fursa na ndiyo maana katika ziara hiyo, rais ameonekana akitembelea katika maeneo ya utengenezaji wa vifaa na vyombo vya bahari, jambo ambalo ni jema.

“Hakika ziara hii itafungua fursa kubwa za ajira kwa kuwa hivi sasa mabaharia wa Tanzania wana soko kubwa nchi za nje, sasa ni wakati wa Watanzania kuchangamkia fursa za masomo,’’ alisema.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akishuhudia utiaji saini wa mikataba ya ushirikiano katika sekta mbalimbali kati ya Tanzania na Ufaransa iliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula, pamoja na Waziri wa Biashara wa Ufaransa, Frank Reicster, katika mji wa Brest nchini Ufaransa, Februari 11, 2022.

Alibainisha kuwa, katika ziara hiyo, Rais Samia pia aliingia makubaliano na Ufaransa kuhusu mambo mbalimbali, hivyo ni muhimu sasa jamii kuandaliwa ili kunufaika na fursa zitakazokuja.

Kwa mujibu wa Dk. Tumaini, sheria ya kimataifa ya bahari imeeleza vyema kuhusu ushirikiano na anachokifanya Rais Samia ni utekelezaji.

“Sasa tumeona mwelekeo bora kwa kuwa Tanzania bara tangu Uhuru hatujawahi kuwa na sera juu ya uchumi wa buluu, huu ndiyo wakati wake kama walivyofanya wenzetu wa Zanzibar kuwa na wizara maalumu,” alisema.

Aliipongeza serikali kwa juhudi inazozichukua katika kutekeleza uchumi wa buluu ili kuwa na tija kwa taifa, ikiwemo kuongeza ajira.

Akifafanua kuhusu mkutano huo, Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa Vijana wa Jumuiya ya Madola kuhusu mabadiliko ya tabianchi, kamati ya sera na utetezi, Delicia Mwanyika, alisema mkutano huo unalenga kuhamasisha jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua madhubuti kulinda uendelevu wa bahari.

Rais Samia alifanya ziara ya kwenda nchini Ufaransa na kuhudhuria mkutano huo wa siku tatu ulioandaliwa na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron na kufanyika Februari 9 hadi 11 mwaka huu.

KANALI LUBINGA

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali mstaafu, Ngemela Lubinga, akizungumzia ziara ya Rais Samia Rais Samia Ufaransa na  Ubelgiji, alisema ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ili kuiwezesha serikali kupanua wigo wa uhusiano kimataifa na kuchochea fursa za uchumi.

“Hii ni fursa ndani ya CCM na taifa kwa ujumla kwa kuwa Ilani imeelekeza serikali kuimarisha uchumi na kuongeza uhusiano wa kimataifa, tumekuwa na uhusiano wa karibu na Ufaransa na Ubelgiji na nchi hizo zote zina ushirikiano wa kiuchumi na Tanzania kwa kuwa wanatumia bidhaa zetu, nasi tunatumia za kwao na kufanya uwekezaji katika miradi mbalimbali,” alisema.

Kanali Lubinga alisisitiza kuwa, CCM inabariki hatua ya ziara hiyo ya Rais Samia ili kuimarisha mifumo kiuchumi na diplomasia, kwa kuwa vyama vya nchi hizo vina mengi ya kujifunza kwa chama tawala cha Tanzania ambacho ni CCM.

Aidha, aliwaondoa hofu wana CCM waliopo katika nchi hizo kuhusu uanachama wao kutokana na kutolewa kwa kadi mpya za kielektroniki, kwa kuwa mifumo inawatambua kupitia matawi yaliyopo chini ya diaspora.

“Hiki ni chama cha umma na tuna matawi nje ya nchi  kupitia diaspora, hivyo wanachama wetu wasihofu, kadi mpya za elektroniki zitawafikia kwa kuwa CCM  hatuna mipaka,”alisema.

MARIAM MZIWANDA Na JUMA ISSIHAKA

Previous Post

MAKUMBUSHO YAKUMBUSHWA KUTUMIA VYEMA FEDHA ZA MIRADI YA UVIKO-19

Next Post

RAAWU YAISIFU SERIKALI KUYAFUNGULIA MAGAZETI

admin

admin

Next Post
RAAWU YAISIFU SERIKALI KUYAFUNGULIA MAGAZETI

RAAWU YAISIFU SERIKALI KUYAFUNGULIA MAGAZETI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Instagram Youtube Twitter Facebook

Browse by Category

  • ! Без рубрики
  • 1
  • 2
  • 231
  • Afya Makala
  • autohenriquesevale.pt
  • best casino
  • Best online casino
  • BIASHARA
  • BURUDANI
  • Business
  • Casino
  • Casino No Deposit Bonus
  • Casino UK
  • casino1
  • casino2
  • casino3
  • casino4
  • curapractic-kerpen.de
  • Forex News
  • gambling platform
  • gambling platforms
  • Gry
  • gry hazardowe
  • HABARI KIMATAIFA
  • Habari Kitaifa
  • Habari Picha
  • Kasyno Polska
  • KIMATAIFA
  • MAGAZETI
  • MAHAKAMANI
  • MAKALA
  • MAKALA AFYA
  • MAKALA-BURUDANI
  • mew casino
  • MICHEZO
  • MICHEZO KIMATAIFA
  • MICHEZO KITAIFA
  • MICHEZO-MAKALA
  • MICHEZO-MASUMBWI
  • MITINDO
  • Nasi Partnerzy
  • new casino
  • niam.cl
  • non gamstop casinos
  • Nos partenaires
  • OM cc
  • Online Casino
  • Online Kasyno
  • Our Partners
  • Partners
  • Post
  • Pozyczki
  • Prestamos
  • Public
  • ready_text
  • RIWAYA
  • sanodelucas.cl
  • SIASA
  • Slots
  • Sports
  • test
  • The best new online casino
  • The best online casino and sportsbook
  • UK Casino
  • Uncategorized
  • Unsere Partner
  • veterinariarepublica.cl
  • wildbeauty.cl
  • www.kuss.cl
  • Микрокредит
  • Наши Партнеры

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved

No Result
View All Result

© 2020 Uhuru Media Group. All rights reserved